KUNA MENGI YA KUJIFUNZA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA SAANANE

Hifadhi ya kisiwa cha Saanane, ilianzisha kama bustani ya kwanza ya wanyama nchini Tanzania 1964. Lengo la kuanzishwa kwa hifadhi hii ya... thumbnail 1 summary

Hifadhi ya kisiwa cha Saanane, ilianzisha kama bustani ya kwanza ya wanyama nchini Tanzania 1964. Lengo la kuanzishwa kwa hifadhi hii ya Saanane ilikuwa ni kuhamasisha uhifadhi na kuelimisha jamii. 
Jina la hifadhi ya Saanane lilitokana na muanzilishi ya bustani alieitwa Saanane Chawandi, kati ya mwaka 1964 na 1966 wanyama mbalimbali wahihamishiwa katika kisiwa hiki ni pamoja na mbogo, digidigi, tembo, pofu, pongo, swala pala, ngiri, pundamilia, kima, twiga, nungunungu, mamba, simba, nyoka .n.k Wanyama wakali kama faru na mbogo walifungiwa na wanyama wapole waliachiwa huru. Bustani hii iligeuzwa kuwa pori la akiba (game reserve) mwaka 1991.

Muonekano wa Ziwa Victoria kutoka katika kisiwa cha Saanane iwapo jijini Mwanza ni kivutio kikubwa sana , Hifadhi hii inaeneo la mita za mraba 0.5, na iko umbali wa km 2 kusini magharibi kutoka katikati ya jiji la Mwanza, katika Ghuba ya Ziwa Victoria. Kisiwa cha Saanane
kinafikiwa kwa boti ukitokea jijini Mwanza. Mtu anaweza kufika jijini Mwanza kwa gari,ndege, treni,mguu na kwa boti.Shunguli za kufanya hifadhini Saanane ni pamoja na kuangalia wanyama, kukwea miamba, kutizama ndege, na safari za kutembea, kupiga makasia kwa kutumia boti, Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Saanane inapitika wakati wote wa mwaka. kwa wanaotarajia kutembea kisiwa cha Sanane kujua garama wasiliana na:

KISIWA CHA SAANANE

S.L.P 11775,Mwanza

simu:+255 28 2541819

barua pepe: saanane@tanzaniaparks.com