MAJANGILI YAKAMATWA NA NYARA ZA MAMILIONI YA FEDHA LINDI

Oparesheni ya kukamata majangili Wilayani Liwale Mkoani Lindi imezaa matunda baada ya kufanikiwa kukamata watu 101 wakiwa na nyara za ... thumbnail 1 summary


Oparesheni ya kukamata majangili Wilayani Liwale Mkoani Lindi imezaa matunda baada ya kufanikiwa kukamata watu 101 wakiwa na nyara za serikali zenye thamani ya sh.212.9 milioni.

Taarifa iliyotolewa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki inaeleza kuwa kati ya watuhumiwa hao tayari kesi 15 zimeshafikishwa mahakamani na moja imeshatolewa hukumu huku kesi nyingine zikiwa katika utaratibu wa kufikishwa mahakani.

Kagasheki alitaja nyara zilizokamatwa kuwa ni pamoja na meno 80 ya kiboko yenye thamani ya sh. 18.8 milioni, meno 14 ya tembo yenye thamani ya sh. 164 milioni na bangili moja ya usinga wa mkia wa tembo yenye thamani ya sh. 23.6 milioni.

Nyara nyingine zilizokamatwa ni ngozi mbili za samba zenye thamani y ash.15.4 milioni, ngozi ya chui sh.5.5 milioni, mikia miwili ya ngedere sh. 378,000, kichwa cha nyati chenye mapembe sh.2.6 milioni na kichwa cha pofu chenye thamani ya sh.2.6 milioni.

Kagasheki alisema mbali na kukamata nyara hizo pia wanashikilia mali za majangiri na vifaa vya ujangili ikiwemo gari aina ya Toyota corona yenye namba za usajili T836 ADV, pikipiki mbili aina ya Sanlg zenye namba za usajili T901 BXQ na T772 BSD, msumeno wa kuchania mbao na mbao 149.

Tabianchi