Exclusive: Wadau wa utalii wataka majangili wauawe, wamwomba Rais aidhinishe jeshi kufanya Oparesheni Uhai kusaka majangili

Umewahi kujiuliza majangili wanaojihusisha na kuua tembo (na wakati mwingine kuua askari wanayampori) huwa wanapatiwa adhabu gani? Adhabu h... thumbnail 1 summary
Umewahi kujiuliza majangili wanaojihusisha na kuua tembo (na wakati mwingine kuua askari wanayampori) huwa wanapatiwa adhabu gani? Adhabu hizo zinatosha ukilinganisha na uharibifu mkubwa wanaoufanya na kulipotezea taifa mapato na nguvu kazi yake.

Mkurugenzi wa Wanyamapori Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Alexander Songorwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa utalii wakati wa maadhimisho ya siku ya tembo kitaifa yaliyofanyika Septemba 22 mwaka huu Mlimani City.

Kupitia majadiliano ya pamoja ya wadau mbalimbali waliohudhuria siku ya tembo kitaifa yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa mikutano wa Mlimani City, Dar es Salaam Septemba 22, 2013 wamependekeza adhabu kali kwa majangili zitungwe.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Jitegemee wakifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa maadhimisho ya siku ya tembo kitaifa
Wadau wa mambo ya utalii wakifuatilia mada wakati wa maadhimisho ya siku ya tembo kitaifa

Katika kipengele kimoja wapo cha mapendekezo hayo kinapendekeza sheria za wanyamapori zijadiliwe upya na bunge na kuingizwa kipengele kitakachoruhusu majangili kuuawa.

Yafuatayo ni mapendekezo 14 ya pamoja kutoka kwa wadau mbalimbali wa utalii ambayo kwayo tunaweza kukomesha ujangili Tanzania

1.   Sheria ziwe kali. Wabunge wajadili upya sheria ya wanayamapori ikiwezekana sheria ya kuua majangili iruhusiwe. 
2.   Mh. Rais apewe taarifa kuhusu hali halisi ya ujangili wa tembo na atangaze kuwa hili ni janga la kitaifa hivyo abariki Operation Uhai irudi tena. Pia atoe agizo kwa jeshi lisaidie katika kupambana na ujangili wa tembo
3.   Ushirikishwaji wa jamii ni muhimu katika mapambano dhidi ya ujangili wa tembo
4.   Idara ya wanyamapori iongezewe nguvu za kifedha na rasilimali watu
5.   Mahitaji makubwa ya matumizi ya teknolojia katika kuhifadhi tembo
6.   Kupambanua na kubainisha aina ya majangili wa tembo waliopo nchini na njia za kukabiliana nao
7.   Bandari zetu zinatakiwa ziwezeshwe kuwa na vifaa vya kubaini meno ya tembo na hata bidhaa zingine wakati zinatoka Tanzania kwenda nchi nyingine. Maana utaratibu wa sasa ukaguzi unafanywa kwenye mizigo inayoingia ndani ya nchi pekee
8.   Ushirikishwaji wa waandishi wa habari upewe kipaumbele ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kifedha na kitaaluma ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa
9.   WMAs zilizopo ziwezeshwe na ikiwezekana zianzishwe nchi nzima
10.               Ushirikishwaji wa wadau mbalimbali katika utafiti wa tembo
11.               Kama mwanachama wa CITES, Tanzania iombe kuwa na mkutano wa wadau wote na kuomba kuwa na ajenda ya kusitisha kabisa biashara ya meno ya tembo
12.               Kuwepo na jukwaa la pamoja katika kupambana na ujangili wa tembo. Ili wadau wakutane wote kupeana taarifa na kupanga mikakati ya pamoja ya kukabiliana na ujangili
13.               Uhimizwaji wa shughuli za kiuchumi ambazo ni endelevu.
14.               IRA kuandaa siku ya tembo kitaifa, mwaka 2014

Endapo mambo haya yakizingatiwa yanaweza kuleta mabadiliko na kupunguza kasi ya ujangili nchini, nap engine ni wakati sasa kwa Rais kuchukua hatua kunusuru tembo wetu na wanyama wengine ambao wako hatarini kutoweka.

Maandhimisho ya siku ya tembo kitaifa, yaliandaliwa na taasisi ya tathmini ya rasilimali ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo, wanasiasa, wataalamu wa mambo ya mazingira na utalii kutoka UDSM, wanafunzi, wanachuo, waandishi wa habari na wadau mbalimbali kwa ujumla wake.
Taasisi hiyo ya Tathmini ya Rasilimali Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IRA) imepewa tena jukumu la kuwa mwandaaji mkuu wa siku ya tembo kitaifa mwaka 2014

www.tabianchi.blogspot.com