Kwa undani: Zifahamu tofauti kati ya Chui na Duma

Si mara moja kukuta mtu akichanganya kati ya wanyama hawa wawili, Chui na Duma (Cheetah) anapowaona kwenye hifadhi mbalimbali hapa nchini.... thumbnail 1 summary
Si mara moja kukuta mtu akichanganya kati ya wanyama hawa wawili, Chui na Duma (Cheetah) anapowaona kwenye hifadhi mbalimbali hapa nchini. leo nimeona nilete kwako tofauti zako ili usiendelee kuwachanganya tena. Kupitia picha na maelezo machache yafutayo utaweza kujifunza kitu.Leopard, I'm sure looking at these photo's you can already spot some differences between them
Chui, naamini kabisa kwa kuangalia picha hii unaweza kubaini alama katika madoa yake mwilini
The slender cheetah. Also notice how the spots are different.
Picha hii pia inatosha kubaini madoa ya duma na umbo lake.

Dondoo:
Chui anaumbo nene na lenye ukakamavu, kwa kuwa ameumbwa kutumia nguvu zaidi katika shughuli zake wakati Duma anaumbo jembamba na refu kwa ajili ya kasi kubwa wakati wa kukimbia.

Chui hufanya mawindo yake nyakati za usiku zaidi wakati Duma yeye huona vizuri zaidi mchana kuliko usiku hivyo uwindaji kwake ni mchana zaidi.

Looking at their faces there is also a difference, the leopard has a stockier face
Uso wa chui

Chui ni mnyama mwindaji anayewinda kimyakimya sana. Ingawa ni mdogo kuliko wanyama wote wa jenasi ya Panthera, chui bado anaweza kuwinda mnyama mkubwa kwasababu ya fuvu lake kubwa lenye taya zenye nguvu.

Ukilinganisha na paka mwili wake ni mrefu zaidi na miguu mifupi na minene, Urefu wa kichwa na mwili wake ni kati ya sm 125 na 165 na mkia wake unakaribia sm 60 mpaka 110.
Urefu wa mabega ni sm 45 mpaka 80. Chui dume ni wakubwa 30% zaidi ukilinganisha na jike, kufikia uzito wa kg 37 mpaka 91 ukilinganisha na jike wenye kg 28 mpaka 60.

Madoa ya chui ni ya mviringo kwa Afrika Mashiriki na huwa ya mraba kwa kusini mwa Afrika wakati chui ana madoa ndani ya miduara midogo kuliko ile ya duma. Chui ni mkubwa na mwenye misuli zaidi kuliko duma.

Chui anafahamika kwa uwezo wake wa kukwea miti, na huonekana akijipumzisha kwenye matawi ya miti wakati wa mchana, akiburuza mawindo yake mpaka juu ya miti na kuining’iniza huko; ingawa, yeye hana nguvu sana kama jamii nyingine ya paka.

Chui naye pia ni mwenye nguvu sana, anaweza kukimbia mpaka km 58 kwa saa, kuruka mbele zaidi ya mita 6 na kuruka juu mpaka kufikia hata mita 3. Chui kiasili ni miongoni mwa wanyama wanaowinda usiku, japo wamerekodiwa mara kadhaa wakiwinda mchana, tena hasa wakati anga likiwa si angavu sana. Wao hutumia muda wao mwingi kulala, aidha juu ya miti, kwenye miamba au kwenye nyasi.

Chui huwinda kwa utegemezi. Ingawa hupendelea wanyama wa umbo la kati, chui hula kitu chochote kuanzia kombamwiko alaye kinyesi mpaka wakubwa pofu dume mwenye kg 900. Milo yao hujumuisha sana wanyama wenye kwato na nyani, lakini rodent, reptilia, amfibia, ndege na samaki nao huliwa pia. Kwa Afrika, swala wa umbo la kati ndio chakula kikuu cha chui, hasa impala na swala wa Thomson.


Chui hunyatia windo lake kimyakimya na dakika ya mwisho kisha kumrukia, humnyonga koo lake kwa kumng’ata haraka. Chui kwa kawaida huficha mawindo yao kwenye vichaka vilivyoshona au huyachukua mpaka juu ya miti, na wana uwezo wa kubeba wanyama hata wenye uzito mara tatu ya uzito wao. 
Chui ndiyo mnyama pekee miongoni mwa jamii ya paka anayeweza kubeba mawindo yake juu ya miti. Uchaguzi wa mawindo kupitia tafiti umeonekana kuzingatia hali fulani ikiwemo ukubwa wa kundi analokuwemo mnyama awindwaye, ukubwa wa pori na mazingira yasiyoweza kuhatarisha maisha ya mwindaji, chui.

The face of the cheetah has the unmistakeable tear marks on it
Uso wa Duma

Duma ni mnyama katika kundi la wanyama walao nyama, yuko katika jamii ya paka. Ngozi yake ni manjano inayoelekea kwenye rangi ya udongo iliyopambwa na madoa meusi. 

Kichwa chake ni kidogo zaidi ukilinganisha na wanyama wengine wa jamii yake kama chui. Wanapokua, madume hutembea peke yao katika kundi duma watatu au wawili.

Wanaungana na majike wanapokuwa kwenye joto tu na sivinginevyo. Rangi ya duma inashabihiana na mazingira yake ya mawindo hutegemea zaidi mbio na kuona ukilinganisha na wanyama wengine wawindaji ambao hutegemea kunusa na kuvizia katika mawindo yao.


Ndiye mnyama anayeaminika kuwa na mwendo kasi zaidi kuliko wanyama wengine watembeao kwa miguu hukimbia kilometa 113 kwa saa. Chakula chake ni wanyama jamii ya swala hupatika Afrika na kidogo sehemu za Asia.

Tabianchi