Meli ikiwa inazama na ikiwa imezungukwa na mitumbwi pamoja na boti ambazo zilisaidia kwenye uokoaji
RIPOTI
ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, iliyochunguza chanzo cha ajali ya mv
Bukoba, inasema usiku wa kuamkia siku ya ajali, meli hiyo ilipakia
abiria kati ya 750 na 800 pamoja na wafanyakazi 37.
Kati
ya hao, 114 waliokolewa wakiwa hai; wakati 391 waliopolewa wakiwa
wamefariki na kuzikwa katika makaburi ya Igoma, nje kidogo ya Jiji la
Mwanza. Miili mingine ilichukuliwa na jamaa kuzikwa kwao. Jumla ya miili
332 haikupatikana.
Kila
mwaka, ifikapo Mei 21, serikali inayosema haina dini, huongozana na
viongozi wa madhehebu ya dini na waganga, kwenda eneo la ajali kufanya
kumbukumbu.
Serikali
ilishitaki aliyekuwa nahodha wa mv Bukoba, Jumanne Rume-Mwiru, (sasa
marehemu), Mkaguzi wa Mamlaka ya Bandari Gilbert Mokiwa; aliyekuwa
Meneja wa Bandari ya Bukoba, Alphonce Sambo, na aliyekuwa Maneja wa
Bandari ya Kemondo, Prosper Lugumila.
Meli ya Mv Bukoba ikiwa inazama.
Kesi
hiyo Na. 22 ya mwaka 1998, ilianza kusikilizwa Mei 14 mwaka 2001.
Miongoni mwa waendesha mashitaka katika kesi hiyo ni Eliezer
Feleshi.Hukumu ya kesi ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu,
Juxton Mlay (sasa mstaafu), Ijumaa, 29 Novemba 2002, majira ya saa sita
mchana.
Washitakiwa
wote walishinda kesi, kufuatia hukumu ya kurasa 118 iliyosomwa kwa
dakika 160 na Jaji Mlay kusema, mv Bukoba ilizama kwa sababu haikuwa na
uwiano wa majini na siyo uzembe wa washitakiwa.
Serikali
iliahidi kukata rufaa; lakini hadi leo majaliwa ya rufaa hiyo
hayajulikani; na baadhi ya washitakiwa wamefariki dunia bila kujua hatma
ya kesi hiyo wala stahili zao.
Kwa
kipindi kirefu, mv Bukoba ilikuwa ‘kaburi’ lenye kuelea katika Ziwa
Victoria. Ilikwishapigwa marufuku kufanya safari kwa kuwa haikuwa na
viwango vya ubora wa kuwa majini.
Makaburi ya Igoma ambako wahanga wa Mv Bukoba walikozikwa
Meli
hii ilijengwa na kampuni ya Kibelgiji; ikazinduliwa 27 Julai 1979. Siku
ya uzinduzi, ilibainika haikuwa thabiti na ilikosa uwiano.
Chanzo: JF