MACHIFU 120, MRISHO MPOTO NA WEMA SEPETU KUNOGESHA TAMASHA LA MTU KWAO ARUSHA

Na Woinde Shizza wa Globu ya Jamii, Arusha Zaidi ya machifu 100 kutoka katika mikoa mbalimbali hapa nchini wanatarajia kushiriki  kati... thumbnail 1 summary
Na Woinde Shizza wa Globu ya Jamii, Arusha
Zaidi ya machifu 100 kutoka katika mikoa mbalimbali hapa nchini wanatarajia kushiriki  katika tamasha la "Mtu Kwao" linalotarajiwa kuanza kutimua vumbi May 15 hadi 20 mwaka huu katika kiwanja cha kumbu ya sheikh Amri Abeid jijini hapa. 
Akiongea na waandishi wa habari jijini hapa Mratibu wa tamasha hilo ambaye ni mkurenzi wa kampuni ya Utamaduni Traning L.T.D Janeth Jonas alisema kuwa tamasha hilo litashirikisha machifu 120 kutoka katika mikoa mbalimbali na makabila mbalimbali ya hapa nchini. 
Alibainisha kuwa nia na dhumuni la kuandaa tamasha hili la mtamaduni wetu ni kuweza kuuenzi utamaduni wa mtanzani ambapo ni kuanzia mavazi ya makabila mbalimbali,vyakula pamoja na ngoma kutoka katika makabila yote hapa nchini.
“Pia katika tamasha hili tumeamua kuwaita machifu mbalimbali l kutoka katika makabila mbalimbali hapa nchini na baadhi ya mchifu ambao watauthuria ni pamoja na chifu kutoka oldmoshi ambaye yeye ameshawasili hapa Arusha kwaajili ya tamasha hili Gerald Mandera ,chifu Gilbert Rugal Isambe kutok a kasulu na wengine wengi wote watakuwepo”alisema Janeth
 Aidha alisema kuwa katika tamasha hili kila mtu atapata fursa ya kuona ngoma kutoka katika makabila mbalimbali pamoja na kuonja chakula cha kila aina cha makabila ya hapa nchini pamoja na nje ya nchi 
Alisema kuwa pia katika tamasha hili zaidi ya vikundi vya ngoma 100 vitatumbuiza pamoja na wasanii mbalimbali akiwepo msanii wa ngoma za utamaduni Mrisho mpoto, Wema Sepetu, kundi la Weusi kutoka Arusha, Jambo Squard, Dogo Janja pamoja na msanii kutoka nchini Kenya Daniel ole Sekuo. 
 Naye mmoja wa machifu ambaye atahudhuria tamasha hilo Chiefu Gerald Mandera kutoka Old Moshi alisema kuwa waandaaji wamefanya jambo jema sana kuanda tamasha hili kwani wao ndio wametambua uwepo wa machifu na wameona umuhimu wao mpaka wameamua kuwakusanya pamoja katika tamasha kama hili. 
 Alisema kuwa sasa hivi serikali nayo inawajibu wa kujipanga vilivyo na kutenga siku maalumu kwa ajili ya kufanya tamasha hili kama jinsi wenzetu kutoka katika nchi zingine wanavyo azimisha siku hii katika tarehe hizi na mwezi huu kila mwaka. 
Aidha alibainisha kuwa kuwakusanya watu mbalimbali kutoka katika tamaduni mbalimbali pamoja na makabila mbalimbali itasaidia kwani inaweza kuwezesha hata nchi kupata vazi la taifa kwani makabila haya yate yanakuja yakiwa yamevaa vazi la ukabila wao na hii itakuwa fursa pekee ya kuweza kuchagua vazi hasili la mtanzanzia.
 “Ni aibu kubwa sana unakuta sisi kama Watanzania hadi leo hii hatuna vazi linaloweza kutuwakilisha sisi kama Watanzania na ukiangalia wenzetu wa n je ya nchi wanamav azi yao ya kiutamaduni ambao ukimuona tu mtu amevaa unajua katoka katika kabila Fulani ,naitanishangaza sana kuona mtu anauzarau utamaduni wake na anauweka mbele utamaduni wa kigeni “alisema chifu Gilbert Isambe akibainisha kuwa hii ni fursa ya watu kuja kujifunza mambo mbalimbali kwa vitendo
 Chifu  Gilbert Isambe akiwa na vazi la kichifu
Chifu  Gilbert Isambe akiongea na vyombo vya habari. Pembeni yake ni mratibu wa tamasha la Mtu kwao Bi. Janeth Jonas