MKUTANO WA USHIRIKIANO WA AFRIKA KATIKA KUHAMASISHA KILIMO RAFIKI NA MAZINGIRA WAFANYIKA MJINI BONN, UJERUMANI

Ushirikiano wa Afrika katika kuhamashjisha kilimo rafiki na mazingira unalenga zaidi katika kuhakikisha usalama wa chakula katika nchi z... thumbnail 1 summary
Ushirikiano wa Afrika katika kuhamashjisha kilimo rafiki na mazingira unalenga zaidi katika kuhakikisha usalama wa chakula katika nchi za Afrika, juhudi za maendeleo katika kusaidia wakulima wadogo wadogo na katika suala zima la kilimo katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Hayo yameelezwa na Bw. Richard Muyungi AMBAE NI MWENYEKITI wa Ushirikiano wa Afrika katika kuhamasisha kilimo rafiki na mazingira, alipokuwa akizungumza na wawakilishi kutoka katika nchi za Afrika pamoja na wafadhili ikiwemo Benki ya Dunia mjini Bonn Ujerumani leo.

Akiiwakilisha Tanzania kama mwenyekiti wa ushirikiano huo, Bwana Muyungi  alisema kuwa, kilimo ndiyo uti wa mgongo wa nchi za Afrika hivyo kuna haj ya kuboresha mifumo mzima wa kilimo unaozingatia matumizi endelevu ya rasilimali ya  ardhi, kujengea wakulima uwezo kuhusiana na kilimo chenye tija, na mwisho wa siku kufanikisha suala zima la usalama wa chakula katika mazingira magumu ya mabadiliko ya tabia nchi.

Bw. Muyungu aaliongeza kuwa, kilimo katika nchi za Afrika ndio chanzo kikuu cha kipato na  ajira na ni muhimu sasa kwa nchi za hizo kujikita katikaa kilimo endelevu na matumizi sahihi ya teknolojia ya kisasa.

Kwa upande mwingine bw. Muyungi alisema kuwa sekta ya kilimo katika nchi za Afrika ipo katika hatari kubwa kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi hivyo hatua za haraka zainatakiwwa kuchukuliwa katika kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa chakula,

Lengo kubwa la Ushirikiano huu ni kuhakikisha kuwa nchi za Afrika zinaongeza tija katika kilimo,  zinazingatia hifadhi ya mazingira na kujengewa uwezo kuhusu kilimo rafiki na mazingira kitakachosaidia kuhimili athari za mabadiliko ya tabia nchi na kupunguza uzalishaji wa gesijoto kupitia sekta ya kilimo..