Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la Rashid Ramadhani (Bonge) (31) Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa
Mjini Mpanda Mkoa wa Katavi anashikiliwa na jeshi la polisWilaya
Mpanda Mkoani wa Katavi kwa tuhuma za kukamatwa na meno ya Tembo vipande
nane vyenye uzito wa kilogramu
14 yenye thamani ya shilingi milioni 45
Kwa mujibu wa
Kamanda wa jeshi la polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina msaidizi mwandamizi Dhahiri Kidavashari mtuhumiwa
huyo alikamatwa hapo mei 20
mwaka huu majira ya saa mbili na
nusu usiku katika nyumba ya kulala
wageni inayoitwa Rex iliyoko
katika mtaa wa Majengo A Mjini Mpanda
Alisema siku hiyo ya tukio mtuhumiwa akiwa na mwenzake mmoja ambae
bado hajafamika walifika kwenye
nyumba ya kulala wa geni hiyo ambayo
alikuwa amefikia Rashid huku wakiwa na mkokoteni
waliingia ndani ya Guest hiyo
na na kutowa vipande hivyo vya meno ya tembo ambavyo
vilikuwa vimeviringishwa kwenye
mfuko wa sandarusi na kuvipakia
kwenye mkomkoteni huo
Alifafanua
kuwa baada ya kuwa wamepakia meno
hayo ya Tembo kwenye mkokoni huo raia wema
ambao walikuwa kwenye eneo
waliweza kubaini kilichokuwa
kinaendelea na ndipo walipotoa taarifa kwa jeshi la Polisi
huhusiana natukio hilo
Kamanda
Kidavashari alieleza baada ya jeshi la polisi kutapa taarifa hizo
kutoka kwa Raia wema waliandaa mtengo kwa kushirikiana na Askari wa
Wanyama piri wa Hifadhi ya mbuga ya Katavi katika maeneo mbalimbali ya
Mji wa Mpanda
Alisema askari
hao walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa Rashid
akiwa na meno hayo ya Tembo
wakati akiwa anasukuma mkokoteni
huo muda mfupi tuu baada ya kuondoka kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni
akiwa analekea kwenye Stendi ya mabasi ya Mpanda na huku mwenzake
aliyekuwa nae awali akiwa ameisha tokomea kusiko julikana
Alieleza baada ya
kufanya upekuzi kwenye mzigo huo ndipo Askari polisi na askari wa Tanapa walipoweza kukuta meno ya Tembo vipande nane
vyenye uzito wa kiligramu 14 vya thamani ya
Tshilingi milioni 45 vikiwa
vimeifadhiwa kwenye mfuko wa sandarusi
Kamanda
Kidavashari alisema upelelezi wa
tukio hilo unaendelea na juhudi za kumsaka mtuhumiwa
aliyekimbia pamoja nakuweza
kubaini kubaini vyanzao na mtandao
wa watu wanahusika
katika biashara hii haramu ya meno ya Tembo
Mtuhumiwa Rashid Ramadhani anatarajiwa
kufikishwa mahakamani wakati
wowote kuhusiana na shitaka linalomkabili
baada ya uchunguzi utakapo
kuwa umekamilika
Mwisho