Picha: Aina 10 ya mavazi ya Kiafrika ambayo unaweza kuvaa katika harusi yako

Nimekuwa nikichunguza sana katika Sherehe mbalimbali hasa hizi za Harusi, ambapo huanza kwa kuagwa kwa Binti na Baadae kuwa na Harusi yen... thumbnail 1 summary
Nimekuwa nikichunguza sana katika Sherehe mbalimbali hasa hizi za Harusi, ambapo huanza kwa kuagwa kwa Binti na Baadae kuwa na Harusi yenyewe, kwa kweli Vijana wanajitahidi sana kutokelezea ki Afrika zaidi siku hizi za karibuni kwa kuvaa nguo ambazo asili yake ni ya hapa hapa Afrika, lakini Pia Mabinti hujitahidi sana kuvaa nguo za Kiafrika hasa wakati wa Kitchen Party pale wanapo wafunda . 

Lakini tatizo linakuja sasa wakati wa Harusi kila mtu anataka kuvaa nguo kama wazungu na kusahau kwamba kuna hizi za Kiafrika ambazo pengine wangevaa zaidi wangependeza zaidi kwa sababu zinaelezea u Afrika kabisa na kuvutia zaidi.

Zifuatazo ni Picha ambazo zinaonesha Dhahili jinsi ambavyo utapendeza katika Harusi yeko endapo utavalia ki Afrika zaidi 
Tazama kwa umakini Bibi na Bwana walivyo pendeza Wamevalia Nguo za kawaida kabisa lakini zenye kiwango cha juu, ukiwatazama hawa wameongezeka uzuri zaidi ni kutokana na haya mavazi yao
 Huu ni ubunifu wa Hali ya Juu tazama Nguo ya Kiafrika ikiwa imefanana kabisa na ua ambalo amebeba
 Wewe unaesoma hii sasa hivi hii kitu hebu tazama kwanza .. na haujaoa wala kuolewa unangoja nini sasa? hawa jamaa wamependeza sana na mavazi yao ambayo yamebuniwa ki Afrika zaidi
 Sio lazima mpaka mvae Shela...
 Hii harusi moja kwa moja itakuwa imefungiwa kijijini lakini pia hawa watu wanaonekana ni wa mjini ingawa hapa wamevalia mavazi yao ya asili ya Kiafrika katika Harusi yao.

 Amependeza hajapendeza?
 Ukiangalia kwa umakini vazi hili la huyu binti lina mambo mengi sana, kwanza ukitazama hapa lina manyoya ya ndege halafu kisha inapendeza sana hapa akikolezea na hii nyeupe ... hebu rudini jamani ambao hamjaoa wala kuolewa hii ni nafasi yenu
 Binti wa Kizungu akiwa ki Afrika zaidi
 Sitii neno
Hebu watazame hawa kuanzia juu mpaka chini nazani na wewe utapata kitu hapa...
 Mwisho Vijana wenzangu ambao bado hamna ndoa hebu ikifika mvae japo kama hawa itakuwa poa sana

Imeandaliwa na Fredy Njeje Blog