Huyu
ni Simba Mdogo ambaye tokea akiwa mdogo alikuwa amevalishwa waya
shingoni na kukuwa nayo mpaka anafikisha Miaka Mitatu hali ambayo
ilipelekea shingo yake kukuwa na kuendelea kuumizwa na waya huo mpaka
alipokuja kuokolewa kwa maana ulikuwa unambana na kuendelea kumchana.
Simba
huyo kwa mara ya kwanza alifanyiwa mawindo ilikuwa ni mwaka 2009 katika
hifadhi ya Taifa ya Mikumi lakini juhudi hizo hazikufanikiwa na ilikuwa
ni zaidi ya Mara saba lilifanyika zoezi la kumkamata bila matumaini
yoyote.
Baada ya miaka
mitatu kupita Shingo ya Simba huyo ilizidi kuharibika kwa msuguano wa
ule waya na kusababisha akose nguvu za kuwinda na wadudu walianza
kumtembelea katika kidonda jambo ambalo lingeweza kumsababishia matatizo
zaidi na hata magonjwa.
Juhudi za kumfuatilia simba huyo ziliendelea na baadaye Simba huyo aliyeteseka sana alikamatwa na kutolewa waya shingoni kisha kufanyiwa Matibabu.
Juhudi za kumfuatilia simba huyo ziliendelea na baadaye Simba huyo aliyeteseka sana alikamatwa na kutolewa waya shingoni kisha kufanyiwa Matibabu.
Kutokana na maelezo ya Mlezi mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mikumi Ndugu William Mwakilema alisema kwamba wakati Simba huyo anakamatwa alikuwa bado ana hali dhoofu na alikuwa hana uwezo hata wa kuwinda tena.
Picha mbalimbali zikimuonesha Simba huyo na jinsi alivyo okolewa.
Hivi ndivyo Shingo ya Simba huyo ilivyo haribika baada ya kukaa na waya wa umeme shingoni kwa muda wa miaka mitatu
Baadhi ya Askari wa wanyama pori wakiwa wanamtoa simba huyo kamba shingoni
Mlezi
mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mikumi bwana William Mwakilema akionesha
waya ambazo alifungwa simba huyo akiwa mdogo na kukuwa nazo kwa Miaka
Mitatu
Picha hiii ikimuonesha Simba huyo aliyekuwa na waya shingoni kwa muda wa Miaka Mitatu sasa amepona.