Wajumbe
wa Baraza la Wakilishi wamepitisha bajeti ya makadirio ya mapato na
matumizi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2014/15
huku ujenzi wa Uwanja wa Ndege ukichukua kiasi kikubwa cha bajeti hiyo.
Hayo
yalithibitika wakati wajumbe wote waliponyanyua mikono kuashiria
kukubaliana na yote yaliyomo katika bajeti hiyo ya Serikali.
Waziri
wa Fedha wa Zanzibar, Omar Yussuf Mzee alishukuru wajumbe hao akisema
atahakikisha upungufu wote uliojitokeza unafanyiwa kazi.
“Haya ni matumizi yetu kwa maana hiyo tushirikiane ili kutekeleza kwa manufaa ya taifa letu,” alisema.
Kutokana
na kupita kwa bajeti hiyo, ni dhahiri sasa Zanzibar itaweza kutumia
kiasi cha Sh707.8 bilioni kwa mwaka wa fedha 2014/15 katika kuendesha
shughuli zake.