Mlezi
wa chama cha wake wa viongozi New Mellinium Women Group Mama Tunu Pinda
akiwongoza wakina mama wenzake kuelekea katika kambi ya Maisha Plus
aliye nyuma yake ni Mke wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali. Wakina mama hao
walifika katika kambi hiyo ili kujionea shughul zinazo fanywa na
washiriki katika maisha Plus iliyopo Bagamoyo Pwani
Mke wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali akiwa na Mlezi wa chama cha wake wa viongozi New Mellinium Women Group Mama
Tunu Pinda pamoja na Katibu wa chama hicho cha wake wa viongozi Mama
Pamela Mathayo wakiangalia shamba la mfano ambalo washiriki wa maisha
Plus wanaliandaa.
Mke
wa Makamu wa Raisi Zakia Bilali akiwasha jiko la gesi ikiwa ni ishara
ya uzinduzi wa mtambo wa gesi inayo tokana na kenyesi cha ng’ombe ambayo
imetengenezwa na washiriki wa maisha plus kulia kwake ni mlezi wa chama
cha wake wa viongozi New Mellinium Women Group Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda wakiwa na wake viongozi wakishuhudia uzinduzi huo ambao umefanyika katika kambi ya Maisha Plus iliyopo wilayani Bagamoyo Pwani Picha na Chris Mfinanga.
Wanachama
wa cha wake wa Viongozi New Mellinium Women Group wakiwa katika picha
ya pamoja na washiriki wa Maisha Plus wa hapa nchini na nnje ya nchi
pamoja nawaandaji. (Picha zote na Chris Mfinanga)
Wakati alipokuwa akiongea na wanakijiji cha Maisha
Plus mama Aisha Bilal alisifu kazi hizo kwani zilitengeneza kwa ubunifu mkubwa
na kuwasisitiza wanakijiji waendelee kufanya hivyo kujiletea maendeleo katika
jamii. Naye Mama Tunu Pinda aliwaeleza wanakijiji kuwa waendelee kuwa mabalozi
wazuri na kuwa mfano wa kuigwa na chachu katika kuleta mabadiliko ndani ya jamii.
Aliongezea na kusema kuwa kuna haja ya Maisha Plus kuwa na eneo kila mkoa na kuwekeza katika miradi endelevu itakayowanufaisha washiriki na jamii kwa ujumla. Sambamba na hayo mama Tunu Pinda, Aisha Bilal na Germin Lukuvi walikabidhi mawadawa 30 yaliyotengenezwa na wanakijiji hao kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo ndugu SamwSalianga.
Kijiji cha Maisha Plus chapata ugeni mkubwa
waliotembelea kjijini hapo kujionea mambo mbalimbali yanayofanyika. Ugeni huo
ulifika kijijini hapo baada ya kumaliza shughulisha ya kusafisha kisima cha
kijiji ili kuwa na uhakika wa maji safi na salama na wengine walikuwa na katika
pilika pilika za mapishi.
Wanakijiji waliwalaki wageni hao kwa shangwe ambao ni
wake wa viongozi wa nchi ngazi za juu akiwemo mke wa Waziri Mkuu mama Tunu
Pinda, Makamu wa Rais mama Aisha Bilal, mama Gervina Lukuvi, Mama Sophia
Kawawa, Mama Mgufuli na wengineo.
Ugeni huu ni mkubwa kwa wanakijiji cha Maisha Plus kwani
hawakutegemea kupata ugeni huo hivyo walifurahi na kupata faraja zaidi pamoja
na kuona kuwa mchango wao unatambuliwa kitaifa na kuthaminiwa na viongozi nchini.
Ugeni huu ulipata fursa ya kutembelea kila kaya kijijiini hapo na kujionea kazi
za ubunifu walizofanya kwa kipindi kifupi cha siku tano ambapo miradi
mbalimbali ya kuvutia iliibuliwa na kuonyesha ujuzi na ubunifu wa hali ya juu
waliokuwa nao wanakijiji hao unaoendana na mazingira yanayowazungka.
Miradi
hiyo ni pamoja na utengenezaji wa sabuni ya aji na kipande, batiki, bustani za
kuhama, aina mbalimbali za majiko yanayotumia kuni chache, kikapu cha ajabu
kinachotunza chakula kisipoe na kuivisha chakula pia, ufugaji bora na wa kisasa
wa kuku na nyuki, jiko la gesi na mengine mengi.
Wakati wa kutembelea
kaya za kijijini hapo alikaribishwa katika familia ya Shida
Keneth Mganga na kupata chakula cha mchana na familia hiyo ingawa hakupendezwa
na jina la hilo na kumpatia jina la TUnu. Vile vile alikabidhi kiasi cha
shilingi 70,000/= kwa Malkia wa kijiji Pendo Mussa kama mchango wao kwa
wanakijiiji hao.
Aliongezea na kusema kuwa kuna haja ya Maisha Plus kuwa na eneo kila mkoa na kuwekeza katika miradi endelevu itakayowanufaisha washiriki na jamii kwa ujumla. Sambamba na hayo mama Tunu Pinda, Aisha Bilal na Germin Lukuvi walikabidhi mawadawa 30 yaliyotengenezwa na wanakijiji hao kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo ndugu SamwSalianga.