Vipi Mlima Kilimanjaro utangazwe na ndege ya Kenya wakati Tanzania ina ndege zake?

Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) ikiwa na jina la Mlima Kilimanjaro. Wiki moja imepita tangu Shirika la... thumbnail 1 summary

Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) ikiwa na jina la Mlima Kilimanjaro.
Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) ikiwa na jina la Mlima Kilimanjaro.

Wiki moja imepita tangu Shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania) lianze safari za visiwani Zanzibar.

Ikiwa ni hatua kubwa kwa shirika hilo ambalo limekuwa na matatizo kiasi ya kushindwa kufanya safari za hata ndani ya nchi ya Tanzania.
Hayo yote yakiendelea jambo la kushangaza ni kuona namna Shirika la Ndege la Kenya (KQ) likiendelea kupiga hatua kwa kununua ndege kubwa zaidi na kupanua safari zake za nje.
Yumkini shirika hilo (KQ) limeweza kutangaza jina la Mlima Kilimanjaro ubavuni mwa ndege hiyo na kitendo kinachotegemewa kuona kinafanywa zaidi na Shirika la Ndege la Tanzania.
Wakenya wanazidi kuchangamkia fursa nyingi Tanzania, watanzania wako wapi?