Watalii wamelazimika kutoa msaada kwa mtoto wa tembo kwa kumpandisha kwenye gari lao baada ya kuonekana amepotea na kuzingirwa na fisi wenye njaa ambao walitaka kumla.
Kikawaida hairuhusiwi kuokoa mnyama kwenye hifadhi za taifa labda iwe ni kwa wahusika wa hifadhi kufanya hiyo kazi wakiona inafaa lakini watalii hawa walilisahau hilo baada ya kujawa na huruma.
Picha zifuatazo zinaonyeshaa baadhi ya matukio ya uokoaji wa tembo huyo mtoto ambaye baadae aliachiwa na kufanikiwa kujiunga na kundi la tembo wenzake.