Mtwara Festival kufanyika Agosti 16-17, 2014 kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara

Bw. Anic Kashasha, Mwenyekiti Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali Tanzania Creative Industries Network (TACIN) ya Dar es Salaam, ... thumbnail 1 summary
Bw. Anic Kashasha, Mwenyekiti Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali Tanzania Creative Industries Network (TACIN) ya Dar es Salaam, nilikuwa ninahutubia mkutano wa waandishi wahabari kwenye ukumbi wa Safari Lounge, mjini Mtwara, juu ya kuanzisha Mtwara Festival, utakaofanyika tarehe 16 - 17 Agosti, 2014 kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona,Mtwara.

Mtwara Festival imeandaliwa kwa kushirikiana na washirika wakuu na wadhamini wa TACIN, Shirika la maendeleo ya Petroli  Tanzania (TPDC). Huu ni mkakati endelevu wa mawasiliano ili kuwahasisha wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi, kuzitambua, kujiandaa na kuzichangamkia fursa zinazotokana na uiwekezaji mkubwa unaendelea katika mikoa hiyo.

Mtwara Festival itakuwa ni tukio la kila mwaka kwa malengo ya kuitangaza mikoa ya Mtwara na Lindi kama mikoa yenye vivutio vingi vya utalii wa utamaduni ikiwa ni pamoja na uchongaji wa vinyago vya na ngoma mbalimbali zenye mvuto Mkubwa. Bodi ya Utalii (TTB) ni Wadau katka mpango huu na watautangaza kupitia njia zake zote yaani mtandaoni, DVD, na majarida yatumikayo kuitangaza Tanzania kwenye Masoko mbalimbali duniani kote. Aidha, TTB wataiweka Mtwara Festival kwenye kalenda ya matukio ya ki- utalii ya Tanzania.

Wenyeji wa Mtwara Featival ni Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara, Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara (V). Chama cha Wafanyaniashara, Wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA) tawi la Mtwara nao ni washirika wa mpango huu.