Na Rashda Swedi- VPO
Viwanda
vitakavyokiuka masharti na kanuni za kulinda mazingira havina budi
kufungiwa mpaka vitakapofuata taratibu na sheria za utunzaji wa
Mazingira, ameseme jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu
wa Rais - Mzingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Mahenge alipofanya ziara
fupi ya kutembelea kiwanda cha kuzalisha mafuta (Murza Oil Mills
Limited) kilichopo Vingunguti.
Dkt
Mahenge alisema hayo baada ya kutoridhishwa na mfumo wa maji taka ya
kiwanda hicho na kuwaambia waboreshe zaidi mfumo wa maji taka kwa lengo
la kulinda mazingira kwa sababu wasipofanya hivyo Serikali itachukua
hatua ya kukifunga kiwanda hicho.
Wakati
huo huo, mwanasheria wa NEMC Bw.Manchale Heche amesema kuwa, kutokana
na ziara waliyoifanya pamoja na Mh. Waziri wamegundua mengi na
hawatafumbia macho suala la viwanda vinavyotumia magogo, kuni na wale
wasiokuwa na mfumo mzuri wa majitaka endapo hawatafuata masharti
waliyokubaliana nayo viwanda hivyo vitafungiwa.
Waziri
alitembelea pia bwawa la maji taka lililopo Vingunguti jijini Dar es
Salaam na kugundua kuwa kuna uharibifu mkubwa wa Mazigira, kutokana na
maji machafu yanayotoka katika viwanda mbalimbali karibu na eneo hilo
kutiririsha maji yao kwenye mabwawa hayo.
Kutokana
na hilo amewataka Manispaa kushirikiana na NEMC kuvijua viwanda
vinavyopitisha maji machafu moja kwa moja bila kufuata utaratibu
uliowekwa.
"Ni
wajibu wa kila mtu kulinda mazingira na sio wajibu wa Ofisi ya makamu
wa Rais tu kwani Mazingira ni yetu sote na ni muhimu kuyalinda" Mh.
Mahenge alisema.Alisisitiza kuwa, huo hautakuwa mwisho wa ukaguzi wa
viwanda utaratibu wa kukagua viwanda utaendelea kuangalia Mazingira
rafiki kwa wananchi.
Meneja
wa kiwanda cha Murza Oil Mills Limited Bw. Dinesh Kana (wa tatu
kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith Satano Mahenge (wa nne kushoto)
kuhusu mfumo wa maji taka ambao wanautumia katika kiwanda hicho.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith
Satano Mahenge akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mazingira wa Wilaya ya
Ilala bw. Abdon Mapunda (wa pili kushoto) alipotembelea bwawa la maji
taka la Vingunguti jijini Dar es Salaam.
Maji
machafu yanayotoka katika viwanda mbalimbali vilivyopo Vingunguti
jijini Dar es Salaam ambayo hutiririsha maji yake katika mto wa
msimbazi, maji ambayo yanahatarisha afya ya binadamu
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Mh. Dkt. Injinia Binilith
Satano Mahenge akipata maelezo kutoka kwa Bw. Richard Matari ambaye ni
msimamizi wa dampo la Kinyamwezi lililopo Pugu jijini Dar es Salaam,
baada ya waziri kuwasili katika dampo hilo na kutaka kujua utendaji wa
kazi zao katika kulinda Mazingira.
Sehemu ya dampo la Pugu Kinyamwezi lilopo jijini Dar es Salaam.