Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Baadhi ya wakazi
wa Kitongoji cha Kashalami Kata ya Mashimboni
wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamelazimika kushinda juu ya miti kwa
kuhofia kushambuliwa na Kiboko
aliyevamia kijiji hicho na
kuhatarisha uhai wa Wanachi
Kwa mujibu wa
Diwani wa Kata hiyo ya Mashimboni
Raphael Kalinga tukio hilo
lilitokea hapo Agos 18 majira ya saa
moja na nusu asubuhi
Akielezea tukio
hilo alisema Kiboko huyo baada ya kuvamia kijiji hicho alielekea
kwenye nyumba ya mkazi mmoja aitwaye Joseph Kashamakula
ambae alinusurika kushambuliwa na Biboko huyo wakati
alipokuwa akitokea chooni kujisaidia
Diwani
Kalinga alisema ndipo Kiboko huyo
ambae alionekana kuwa na hasira
alipoanza kukanyaga kanyanga na vuvivunja vyombo vya mwanakijiji
huyo ambavyo vilikuwa nje ya nyumba yake
na kuviharibu kabisa hari ambayo
ilimfanya wananchi huyo apige mayowe ya
kuomba msaada kwa majirani
Majirani walifika
kwenye eneo hilo hata hivyo
walilazimika kutimua mbio baada ya kiboko huyo kuanza
kuwafuata hari ambayo ilipelekea kukimbia na kisha kupanda juu ya miti kwa
kuhofia kushambuliwa na mnyama huyo ambae aliendelea kuvunja vyombo kwenye
nyumba mbalimbali
Alisema
Kiboko huyo aliendelea kuzunguka kwenye eneo la kijiji hicho na taarifa za
zilifika kwenye Idara ya Maliasili ya Halmashauri ya Nsimbo
ambao walituma Akari wao wa
wanyama pori kwenda huko
Baada ya Askari wa Maliasli kufika kijijini hapo walianza msako wa kumtafuta kwa kushirikiana
na wananchi ambapo walifanikiwa kumwona
na kisha walimuuwa kwa kumpiga
Risasi tumboni na kichwani
Diwani Kalinga
alieleza baada ya Kiboko
kuuwa wananchi licha ya hapo awali kumkimbia kiboko
huyo walianza kugombea
nyama ya mnyama huyo
kwa kuchukua kitoweo cha mboga
na baada ya nusu saa wakawa wamemmaliza