Ruben Ramirez mwenye miaka 41 ameamua kujitolea kuingia porini huko
Florida, Marekani kupambana na nyoka wakubwa ambao walivamia eneo hilo
tangu mwaka 2000 na kula wanyama mbalimbali katika maeneo hayo.
Ramirez ambaye ni mwenyeji wa eneo hilo ameeleza kuwa wakati anakuwa,
yeye na baba yake walikuwa wakienda porini kuangalia wanyama mbalimbali
lakini tangu chatu hao walipovamia eneo hilo hawaoni tena wanyama hao
na ndio sababu akaamua kuwapunguza.
Mwanaume huyo hupigana mieleka na chatu hao na kuwashika wakiwa hai
kisha kuwakabidhi kwa maafisa wa wanyama pori wanaowatoa katika eneo
hilo kwa lengo la kusaidia wanyama kukua.
Ramirez anaeleza kuwa tayari ameshang’atwa zaidi ya mara mia au elfu
kadhaa na nyoka hao wakati akipapambana nao lakini ameweza kupona kwa
kuwa wengi huwa hawana sumu.
Pamoja na hatari kubwa anayokabiliana nayo, anadai kuwa hufurahia sana kupigana mieleka na nyoka hao.
Angalia Video hapa: