Kundi la kigaidi la Jund al-Khilifa limemuua kwa kumchinja
mtalii wa Ufaransa ikiwa ni sehemu ya ahadi yao kwa nchi hiyo ikiwa
haitasitisha mashambulizi dhidi ya kundi la ISIS nchini Iraq.
Jumapili iliyopita, kundi hilo liliweka YouTube video inayoonesha
wapiganaji walijifunga kitambaa usoni wakimfanyia tukio hilo mtalii
aliyetajwa kwa jina la Herve Gourdel mwenye umri wa miaka 55,
waliyemteka alipokuwa nchini humo.
Ufaransa imeungana na Marekani katika kampeni ya kushambulia kundi la ISIS lililoteka sehemu kubwa nchini Iraq na Syria.