Mabadiliko ya hali ya hewa yamekuwa
yakileta madhara duniani ,nchini Tanzanian mamlaka ya hali ya hewa
imelazimika kutoa taarifa maalumu kwa umma kuhusiana na tahadhali ya
mabadiliko ya hali hewa katika ukanda wa Pwani kutokana na kuimarika kwa
mgandamizo mdogo wa hewa katika eneo la Bahari ya hindi mashariki mwa
kisiwa cha Madagascar hali inayoleta mawimbi makali.
Shughuli ya
uvuvi katika bahari ya Hindi ni tegemeo kwa uchumi na huduma ya
samaki,lakini kwa sasa mambo yamebadilika samaki wanapatikana kwa tabu
kufuatia wavuvi kuogopa kuingia Baharini kuvua,huku hali ya usafiri kwa
vyombo vya majini ndani ya Bahari hiyo vikikumbwa na hali mbaya kutokana
na mawimbi makali.
Hali hiyo ya kuchafuka kwa bahari na hali ya
hewa, pamoja na mawimbi makali bahari ya Hindi, ni kilio kikubwa kwa
wavuvi wa mwambao huo wanaoendesha maisha yao kwa kutegemea uvuvi, kwani
kwa sasa samaki hawapatikani tena kama hapo awali.
Hali ya mabadiliko ya tabia nchi, kwa mwaka huu wa 2015 limekuwa si
jambo la kawaida, kwani kwa kawaida nchini Tanzaia majira kama haya ya
mwezi wa kwanza mpaka wa pili katikati upepo hukata na kuwapa fursa
wavuvi kutafuta riziki zao.
Kutokana na mabadiliko hayo ya hali ya
hewa,imeathiri upatikanaji wa mazao ya samaki na sasa bidhaa ya samaki
imepanda bei kutoka elfu kumi ama ishirini kwa ndoo ya lita kumi hapo
awali sasa inauzwa kwa elfu sabini kwa dagaa mchele, na hivyo kumfanya
mjasiriamali mwenye kipato cha chini kutomudu kununua bidhaa hiyo.
Chanzo: BBC