MHE. NYALANDU ‘’TUTAFAKARI TUNAFANYAJE KUWALINDA WANYAMAPORI’’

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu, amesema Wanyamapori ni moja kati ya rasilimali muhimu inayotoa mchango mkubwa kiuchu... thumbnail 1 summary
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu, amesema Wanyamapori ni moja kati ya rasilimali muhimu inayotoa mchango mkubwa kiuchumi, kijamii na kimazingira hapa Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.
Amesema kwamba hadi kufikia sasa ni mataifa machache yaliyobakia yenye wanyamapori wanaopatikana katika mazingira yao ya asilia kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu, uharibifu wa mazingira, kukinzana kwa shughuli za uhifadhi na kiuchumi (viwanda), mabadiliko ya tabia nchi.

Waziri waWizara ya Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Bw. Herman Keraryo akizungumza na baadhi ya Watumishi wa Wizara( hawapo pichani) kwenye maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori Duniani yaliyofanyika jana Mpingo House jijini Dar es Salaam. Mwingine ni Mkurugenzi msaidizi Rasilimali watu, A.R Matagi
 
Akizungumza na Watumishi wa Wizara pamoja na Waandishi wa Habari kwenye maadhimisho ya Siku ya Wanyamapori Duniani yaliyofanyika jana kitaifa jijini Dar es Salaam, Mhe Nyalandu amesema kila mmoja lazima atafakari anafanyaje kuwalinda wanyamapori.
Maadhimisho ya siku ya wanyamapori duniani hufanyika kila tarehe 3 ya mwezi Machi, na nchi mwananchma wa CITES.
Mhe. Nyalandu alisema jamii lazima ilinde na kuhifadhi wanyamapori kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho”.
‘’Tanzania inakabiliana na changamoto kubwa ya ujangili pamoja na biashara haramu ya meno ya Tembo na na pembe za Faru tushirikiane Kutokomeza vita dhidi ya ujangili’’ Mhe. Nyalandu alisisitiza
Alisema kuwa Ujangili unahatarisha maisha ya tembo, ujangili na biashara haramu ya nyara huathiri uchumi wa nchi, ustawi wa siasa, mifumo ya kiikolojia na usalama wa nchi.
Aliongeza kuwa endapo wanyamapori hawa watapungua au kupotea Tanzania itaanguka katika utalii ambao kwa kiasi kikubwa hutegemea Wanyamapori.

Alisema kuwa ili kukabiliana na ujangili na biashara haramu ya nyara za tembo na faru serikali imeamua kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa Idara ya wanyamapori kwa kuunda Mamlaka ya Uhifadhi Wanyamapori Tanzania “Tanzania Wildlife Management Authority-TAWA”
Aidha, Mkuju River Uranium Mining Company (Mantra)” imekabidhi magari mawili aina ya Landcruiser kwa Wizara ikiwa ni jitihada za kuunga mkono kusaidia askari wanyamapori kufanya doria katika mapori nchini