UNESCO: Maendeleo endelevu hayatapatikana bila kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi

Mwakilishi wa Ufaransa katika UNESCO, Jean-Pierre Poncet akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa mkutano m... thumbnail 1 summary
IMG_8112Mwakilishi wa Ufaransa katika UNESCO, Jean-Pierre Poncet akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa mkutano maalum uliofantika leo makao makuu ya UNESCO, Paris, Ufaransa

RoadToParis with tabianchiblog&CFIMedias21
Mwakilishi wa Ufaransa katika UNESCO, Jean-Pierre Poncet amesema kuwa, Maaendeleo endelevu hayatapatikana bila kutatua changamoto za mabadiliko ya tabianchi ambayo yanazikumba nchi nyingi duniani ikiwemo Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Mwakilishi huyo ameeleza hayo leo Julai 6, wakati akizungumza na waandishi wa habari za mazingira kutoka Tanzania, Kenya, Madagascar na Rwanda wanaoshiriki kwenye mkutano mkuu wa wanasayansi juu ya tabianchi ‘Our Common Future Under Climate Change’ unaotarajia kuanza rasmi Julai 7-11, katika makao makuu ya UNESCO, jijini Paris, Ufaransa.

Anasema kuwa, ili nchi ziwe na maendeleo, suala la kupambana na mabadiliko ya tabianchi ni muhimu kuweka mipango madhubuti yatakayoendana na mipango yao ya maendeleo.

Kuelekea katika mkutano mkuu wa 21 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Mabadiliko ya tabainchi (COP 21) utakaofanyika mwanzoni mwa mwezi Desemba mwaka huu, Paris.

Anasema kuwa ili kuleta maedeleo na kupambana kwa vitendo, ni wajibu kwa mtaifa kutoa 
mchango wao katika juhudi za dunia za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi (Intended Nationally Determined Contributions – INDCs). 

Waandishi wanaoshiriki katika mkutano huo wa wanasayansi unaotarajia kuanza kesho, awali ndani ya mwezi Juni, walipatiwa mafunzo ya wiki mbili Nairobi, Kenya juu ya mabadiliko ya tabianchi chini ya mradi wa Media 21 Project.
DSC_1489Mwakilishi wa Ufaransa katika UNESCO, Jean-Pierre Poncet akiwa katika mkutano na waandishi wa habari
DSC_1483Mwakilishi wa Madagascar, mwanahabari/blogger, Lalatiana Rahariniaina akiwa katika pozi... nje ya eneo la kuingilia ukumbi wa mikutano ambao unatarajia kuanza kuanzia Julai 7-11, UNESCO, Paris.DSC_1478Mwandishi wa mtandao wa habari wa modewjiblog.com, Andrew Chale akiwa katika eneo la kuingilia kwenye mkutano katika makao makuu ya UNESCO, Paris tayari kwa mkutano unaotarajia kuanza kesho Julai 7-11.

Chanzo: Moblog