RoadToParis
with tabianchiblog&CFIMedias21
Waswahili
husema usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Umuhimu wa nuru katika giza ni sawa
sawa na umuhimu wa tafiti za wanasayansi katika kupata ufahamu na uvumbuzi wa
mambo mbalimbali katika jamii.
Wanasayansi
wamekuwa na mchango mkubwa sana katika kutafiti na kuibua majawabu ya mambo
mbalimbali ambayo jamii ya watu imekuwa haina ufahamu nayo.
Sehemu ya wanasayansi wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa siku Julai 7, 2015 (Picha na tabianchi blog) |
Julai 7,
2015 wanasayansi zaidi ya 2000 kutoka nchi mbalimbali ulimwenguni wamekutana
kwenye mkutano wa wanasayansi (Our Common Future Under Climate Change) mjini
Paris, Ufaransa kwa lengo la kutoa tathmini ya hali ya mabadiliko ya tabianchi.
Malengo
mengine ni pamoja na kutafuta njia za kukabliana na mabadiliko ya tabianchi kama
njia ya kuelekea kwenye kufikia makubaliano ya mkataba mpya wa mazingira hapo
desemba mwaka huu wakati wa Mkutano wa ishirini na moja wa nchi wanachama wa Mabadiliko
ya Tabianchi COP21.
Wanasayansi
hawa wanajadili na kupima ushahidi wa mabadiliko ya tabianchi ambao umekuwa
ukitolewa kupitia tafiti mbalimbali ili kutoa fursa kwa jamii kujua na kujadili
mambo ya kisayansi yanayogusa maisha yao.
Mkutano huo ambao
unafanyika kipindi kifupi baada ya ripoti ya tano (AR5), ya jopo
la kimataifa kuhusu Mabadiliko ya tabianchi (IPCC), pia utatoa
nafasi kwa wadau na wanasayansi kujadili majawabu ya namna ya kupunguza na
kuzuia mabadiliko ya tabianchi.
Maeneo
ambayo yanajadiliwa ni pamoja na elimu ya maendeleo endelevu, sayansi, sera na
jamii, mambo ya bahari na hali ya hewa, maji salama na elimu ama ufahamu kwa
watu wa maeneo ya vijijini.
Mkutano huo
umeandaliwa chini ya mwamvuli wa ICSU, Future Earth, UNESCO, taasisi za utafiti
za Ufaransa na kufadhiliwa na serikali ya Ufaransa.