Mgeni rasmi Kaimu
Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya
Maliasili na Utalii, Gladness Mkamba akizungumza na wadau wa maliasili
pamoja na waandishi wa habari ,ambapo alisisitiza kulinda misitu kwani
uvunaji umekuwa mkubwa nahivyo kupelekea ukame katika nchi yetu pia
alisisitiza kutoa elimu kwa jamii inayozungukwa na misitu hiyo katika uzinduzi wa kampeni ya mfululizo wa
vipindi vipya vya runinga pamoja na uzalishaji endelevu wa mkaa
vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali za hapa nchini Tanzania
Msaidizi wa Balozi, Ubalozi wa Ufini(Finland) ambao ni wafadhili wa Mama Misitu, Simo-Pekka Parviainen akizungumza jambo katika uzinduzi wa kampeni ya mfululizo wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini
Mkurugenzi
wa Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF), Joseph Olila akiwasisitiza
waandishi wa habari kutumia nafasi hiyo kwa ajili ya kutoa elimu kwa
jamii na hata kufikisha ujumbe ulio sahihi kwa jamii.
Mkurugenzi
Mtendaji Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA),
Rahima Njaidi akitoa somo kwa wadau wa maliasili hasa katika uvunaji wa
misitu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya mfululizo wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini
Mkuu wa Mradi ya Kilimo, Kipato na Ajira wa Shirika la Maendeleo la Uswisi, Ueli Mauderli akitoa neno katika uzunduzi wa Kampeni ya kipindi cha Tv
Mshauri wa Ufundi Wizara ya Maliasili na Utalii, Thomas Sellaine akizungumza jambo katika uzinduzi wa kampeni ya mfululizo wa
vipindi vipya vya runinga vinavyo kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa
vitakavyo kuwa vikirushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini
Balozi wa Mama Misitu, Asha Salimu (kushoto), akizungumza jambo katika uzinduzi huo.
Meneja Kampeni Mama Misitu, Gwamaka Mwakyanjala, akizungumza katika uzinduzi huo.
Mwezeshaji, Faustine Ninga(wa kwanza kulia) kutoka Taasisi ya Natural Resource Forum (TNRF) akizungumza jambo
Kaimu
Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki katika Wizara ya Maliasili na
Utalii, Gladness Mkamba ambaye alikuwa ni mgeni rasmi akibonyeza kwenye
kopyuta mpakato kudhihirisha ufunguzi rasmi wa kampeni ya mfululizo wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa, ambavyo vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini
Wadau wa mazingira pamoja na waandishi wa habari wakiwa katika mkutano
Picha ya Pamoja
MFULULIZO
wa vipindi vipya vya runinga kuhusu uzalishaji endelevu wa mkaa
vitarushwa hewani kupitia televisheni mbalimbali nchini. Kampeni ya Mama
Misitu (MMC), inazindua mfululizo wa vipindi vya kuelimisha jamii
kuhusu uzalishaji na faida za mkaa endelevu kijamii, kimazingira na
kiuchumi.
Vipindi
hivyo mfululizo vimetengenezwa katika wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro
ikiwa ni sehemu ya jitihada za pamoja kati ya Mtandao wa Jamii wa
Usimamizi wa Misitu Tanzania (MJUMITA), Shirika la Kuhifadhi Misitu ya
Asili Tanzania (TFCG), Shirika la Kuendeleza Teknolojia za Asili
(TATEDO) na Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa ili kuleta mabadiliko na
kurasimisha sekta ya mkaa iweze kutoa ajira endelevu na kipato kwa jamii
za vijijini na mijini.
Inakadiriwa
kuwa mkaa na biashara za kuni huzalisha takriban (dola bilioni 1) za
mapato kwa zaidi ya wazalishaji, wasafirishaji na wafanyabiashara laki
tatu (300,000) katika mwaka 2012. Mahitaji ya mkaa nchini Tanzania
yameongezeka kwa kasi na kwa kiasi kikubwa.
Mkaa
endelevu ni mkaa unaozalishwa kwa njia endelevu kutoka katika Misitu ya
Hifadhi ya Jamii bila kuchangia ukataji miti na uharibifu wa mazingira.
Hata hivyo, uzalishaji wa aina hii ya mkaa bado haujajulikana. Kampeni
hii mpya ina lengo la kuleta mabadiliko kupitia ubunifu wa vipindi
mfululizo vya runinga ambavyo vinazinduliwa leo.
Nishati
zitokanazo na tongamotaka (biomas) ni nishati muhimu sana nchini
Tanzania itakayoendelea kutumika angalau zaidi ya miaka 20 ijayo. Kwa
sasa, mkaa mwingi huzalishwa kinyume na utaratibu kutoka katika misitu
ya hifadhi na misitu ya vijiji isiyo na mipango ya matumizi endelevu.
Kutokana na usimamizi hafifu wa uzalishaji wa mkaa, imesababisha ukataji
miti na uharibifu wa misitu kuongezeka nchini Tanzania.
Kampeni
ya Mama Misitu na washirika wake (TFCG na MJUMITA) inalenga kuleta
mabadiliko katika sekta ya mkaa kutoka tatizo kuwa fursa kubwa muhimu.
Hivyo, vipindi vya runinga vya Mama Misitu pamoja na jumbe muhimu za
mawasiliano zitasambazwa nchini Tanzania ili kuibua mjadala wa pamoja
juu ya kuboresha utawala bora wa rasilimali misitu na kuleta faida kwa
watanzania.
Mama
Misitu ni kampeni ya mawasiliano yenye lengo la kuboresha utawala bora
wa misitu ya Tanzania na kupunguza uvunaji haramu wa mazao ya misitu ili
watu wa Tanzania wanufaike zaidi na rasilimali misitu zao.