Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
Shirika
la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) pamoja na
Kampuni ya TOSHIBA ya nchini Japan zimetiliana saini Mkataba wa
Maelewano wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria
vya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi.
Utiaji
saini wa mkataba huo umefanyika Desemba 4, 2015 Jijini Dar es Salaam
katika Ofisi za TGDC ambapo hatua hiyo itaiwezesha TGDC kuweza kupata
msaada wa kitaalam ambao utaliwezesha shirika hilo kuweza kuchimba
ardhini kwa lengo la kupata mvuke utakaoweza kuzalisha umeme.
Akiongea
ofisini kwake, Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe amesema
kuwa kupitia Serikali ya Japan hususani Shirika la Maendeleo Japan
(JICA), Kampuni ya TOSHIBA watasaidia kuomba ufadhili wa Serikali yao
ili kuweza kuendeleza ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme pamoja na
matumizi mengine yanayoendana na nishati hiyo.
“Katika
utafiti wa nishati ya jotoardhi tunahitaji watu wenye elimu na uzoefu
na ujuzi wa kutosha, miongoni mwa makubaliano ndani ya mkataba huu
tuliosaini leo ni wafanyakazi wetu kadhaa kuwapeleka nchini Japan kwenye
vyuo vyao ili kuweza kupata mafunzo ya darasani na kutembelea maeneo
ambayo Japan wana vituo vya jotoardhi ili wapate ujuzi wa kufanya kazi
na Wajapan na kutuletea ujuzi huo hapa nchini”, alisema Njombe.
Aidha,
ameeleza kuwa kupitia ushirkiano huo na Serikali ya Awamu ya Tano Japan
itaendelea kuisadia Tanzania katika kuendeleza nishati ya jotoardhi
kwakuwa ni nishati yenye tija katika kutimiza ndoto za Tanzania kwa
kuifanya kuwa nchi yenye kipato cha kati kufikia mwaka 2020.
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi
Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu
toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakiweka saini Mkataba wa wa
Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya
upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es
Salaam.
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi
Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu
toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakikabidhiana Mkataba wa
Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya
upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es
Salaam.