Dotto Kahindi, Paris,
Ufaransa
Desemba 9, 2015, Rais
wa Mkutano
wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi COP21, Manuel Pulgar-Vidal ametoa andiko la kwanza la Mkataba
wa Mabadiliko ya Tabianchi baada ya majadiliano makali baina ya nchi zilizo
wakilishwa kwa mkutano huo.
Mkataba huo
unatarajiwa kupitishwa wiki hii baada ya kufikia makubaliano ambayo hata hivyo
yanaonekana kuwa na ukakasi katika kuyafikia.
Baada ya kulipitia
andiko la mkataba huu nimekuandalia mambo 7 ambayo yanahitaji kurekebishwa
kabla ya kuingia makubaliano ya mwisho yatakayofanya andiko hilo kuwa shuruti
kwa kila nchi mwanachama.
Utangulizi
Katika sehemu ya
kwanza ya Mkataba huo inaanza kutumika lugha nguvu na inayojificha, jambo
ambalo « linaweka upenyo wa nchi zilizoendelea kukwepa majukumu yao.
« Kwa mfano
kwenye andiko kunakipengele kinachosema, nchi itasaidia kulingana na hali
yake ya kiuchumi kwa wakati huo. Kipengele hicho kinapaswa kuondolewa »
anasema Fazal Issa Afisa Mirafi ForumCC
Nchi zinazoongoza kwa
kuzalisha hewa ukaa kuwa na wajibu wa kusaidia nchi zinazoendelea kwa kuwa wa
kwanza badala ya kuacha mzigo kwa nchi zinazoendelea.
Wastani wa joto
Asasi nchi nyingi
zinataka wastani wa joto uwe 1.5 nyuzi joto, tofauti na inavyoonekana sasa kwa
mataifa yalioendelea kutaka nyuzi joto 2. Kwenye andiko la sasa bado inaonyesha
mambo yote mawili, ikiwa ni nyuzi joto 1.5 na nyuzi joto 2. Ni muhimu jambo
hili kuamuliwa na kupata msimamo mmoja hasa ule unaoungwa mkono na watu wengi
na wenye uhalisia ambao ni nyuzi joto moja na nusu.
Upunguzaji wa gesi
Joto.
Fazal Issa anasema Tunataka
kwamba mwaka wa kuanzia kupunguza gesi joto uanzia mwaka 1990 badala ya 2010 kama
ilivyoandikwa katika andiko hili na kwa asilimia tunataka 75% katikati ya karne
na 100% mwisho wa kanrne »
Kuna haja pi aya
kuwepo kwa masharti ambayo yatahakikisha nchi zilizotoa ahadi zitekeleze ahadi na
ili kufanikisha hilo nchi zilizoendelea zisisimamiwe bali zijisimamie zenyewe
kufikia nyuzi joto hizo.
Kukabiliana na
mabadiliko ya tabainchi
Juhudi zote zilenge
katika kufikia kwenye nyuzi joto 1.5 na sio kama inavyoonekana hapa kwenye
andiko hili la mkataba. Ikiwa ni pamoja na kiwango cha fedha ya misaada
kiongezeke.
Inapaswa kuwa na
uwazi mpana maana kwa andiko hili hakuna kilichoandikwa kwa tarakimu kuwa nchi zilizoendelea
zitatoa kiasi gani cha fedha za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Andiko hili
limetambua umuhimu wa nchi zilizoendelea kutoa misaada kwa nchi
zinazoendelea. Lakini hawatakiwi kuishia
kutoa usaidizi tu bali kutambua kuwa ilo ni jukumu na wajibu wao.
Uharibifu na
upotevu
Katika andiko hili
bado hawajatambua kama jambo hili linaweza kuwa na ibara yake inayojitegemea
lakini ni muhimu jambo hili liwe kwenye ibara yake inayojitegemea.
Kwa sababu toka
Poland COP19 walikubaliana jambo hili ni muhimu, ni zaidi ya kukabiliana na
mabadiliko ya tabianchi na hivyo ni
vyema likasimama kwenye kipengele kingine badala ya kuliunganisha na mambo
mengine.
Fedha za
mabadiliko ya tabianchi.
Andiko hili limeficha
mambo mengi kwenye mabano ambayo ndio hasa yanahitajika, haionyeshi ni kama
fedha hizo zimeongezeka na kama zinatabilika zinakuja lini, kwa kiwango
kinachotakiwa na kama zinapatikana kwa
njia rahisi.
Mfumo wa taasisi
na kuanza kwa mkataba huo
Baada ya majadiliano
ya Paris kumalizika, Katibu Mkuu wa COP atawaalika wanachama wote Aprili 22,
2016 ili kutia sahihi mkataba huu na utakuwa wazi kuridhia mpaka 2017.
Jambo ambalo haliko
sawa hapa ni idadi ya wanachama wanaotakiwa kuasini ili kuupa nguvu ya kuanza kutumika
mkabata huo ni 50 au 60 lakini kwa utaratibu wa kupata theluthi moja ya
wanachama 196 namba inayokuja ni 65. Hivyo kuna haja ya andiko hilo kuonyesha
idadi ya wajumbe 65 badala ya 50 au 60 inavyoonyesha sasa.
Jambo jingine ni lile
la kunakujitoa kwa wanachama, ambapo mwanachama anaweza kuandika barua kwa
katibu na kujitoa kwenye makubalinao na mkataba huo baada ya miaka mitatu,
jambo hili linaweza kuondoa nguvu ya utekelezaji wa makubaliano hayo kwani nchi
inaweza kujitoa kwa kushindwa kutekeleza wajibu wake.
Ni vyema kuwa na
kipengele kitakachowezesha kufanyika kwa uchunguzi kubaini sababu za msingi
zilizosababisha nchi husika kujitoa kwenye mkataba huo.
Ni hayo kwa sasa,
tuendelee kusubiri andiko la mwisho la mkataba huu ambalo linatarajiwa kutoka
kabla ya saa 24 kuanzia sasa.