Rais Magufuli akiwa anaongea na wananchi wa eneo la Mbauda lililopo ndani ya jiji la Arusha
Na Woinde Shizza,Arusha
Msafara
wa Rais John pombe magufuli uliokuwa ukielekea Monduli mapema leo
umesimamishwa na wananchi katika eneo la Mbauda lililopo ndani ya jiji
la Arusha ili kushinikiza kutatua kero zao na changamoto zao ikiwemo
kuwepo na kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Mount Meru Mill
kinachodaiwa kuchafua mazingira na kuhatarisha afya za wakazi wa eneo
hilo.
Wananchi
hao ambao walijikusanya kuanzia mida ya saa mbili kamili asubui mbali
na kumueleza Rais huyo kero zao, pia walitumia nafasi hiyo kumpongeza
kwa kazi anayofanya na kumuomba aendelee kutumbua majipu yaliyopo humu
nchini.
Akiongea
mbele ya Rais mara baada ya kupewa nafasi , mmoja wa wanachi wa eneo
hilo la mbauda Thabiti Abubakari alimuomba rais awasaidie kutatua
tatizo la kiwanda hicho kutiririsha maji machafu ya kiwandani kwani
tatizo hilo ni baya na linawaharibia mazingira na kuhatarisha afya zao .
‘’Musheshimiwa
rais tunapenda utusaidie hapa kwetu mbauda tuna kero kubwa inatusumbua,
kuna hiki kiwanda cha mafuta ya kupikia cha mount meru mill kimekuwa
kinatiririsha maji machafu ya kiwandani huku nje ambapo wananchi
wanaishi , kiwanda hiki hakijajenga mitaro ya kupitisha maji machafu
hivyo maji yote machafu yakitoka huko kiwandani yanaingia huku majumbani
kwetu, hivyo muheshimiwa tunaomba utusaidie hili tatizo kwani kiwanda
hiki kipo ndani ya makazi ya watu,kinahatarisha afya sasa
inatuatarishia afya zetu pamoja na za watoto wetu ambao wanacheza uku
mitaani pia tunaweza kupata magonjwa ya milipuko kama kipindupindu maana
maji haya ni machafu sana”alisema Dhabiti
Akijibu
swala hilo Rais magufuli alisema kuwa amelisikia na aliwaagiza mamlaka
ya usafi wa mazingira nemc kulifuatilia swala hili mara moja .
Aidha
magufuli alitumia muda huo kuwashukuru wananchi wa jiji la Arusha kwa
jinsi walivyoendelea kujitokieza kumpokea na kuwahaidi ataendelea
kutekeleza yale yote aliyoyahaidi katika kipindi alipokuwa akifanya
kampeni.
Alisema
kuwa kipindi hiki akuja arusha kwa ajili ya kuongea na wananchi hivyo
basi ataandaa siku na kuja rasmi arusha kufanya mkutano mkubwa ambao pia
atatumia mda huo kusikiliza kero za wananchi wa jiji la hilo.
Chanzo: Michuzi blog
Chanzo: Michuzi blog