Gereza la Keko latozwa faini Mil 30 huku kiwanda cha dawa keko kikitozwa faini Mil 20 kwa uchafuzi wa mzingira

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akizungumza na waandishi wa habari mapema hii jana mara b... thumbnail 1 summary
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akizungumza na waandishi wa habari mapema hii jana mara baada ya kufanya ziara ya ukaguzi wa mazingira jijini Dar es salaam.       
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akikakagua uchafuzi wa mazingira unaofanywa na gereza la keko lililopo temeke jijini Dar es salaam.        
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akifanya akipita pembezoni mwa mfereji wa maji taka, ambapo uko karibu na makazi ya watu

 Kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Naibu Waziri Ofisi ya makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina (Mb.) Amelitoza faini ya shilingi milioni thelathini  Gereza la keko kwa kosa la kutiririsha maji taka yanayozalishwa gerezani hapo  hivyo kuhatarisha maisha ya Binadamu na viumbe hai wengine.
Akiwa katika ziara nyingine ya ukaguzi wa mazingira jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri Mpina Alilitaka Baraza hilo kutoa agizo kwa mkuu wa gereza hilo litakalokuwa na maelekezo ya  kujenga miundombinu ya majitaka ambayo ni rafiki kwa mazingira sambamba na kulipa faini hiyo kwa muda uliyotajwa.

“Taasisi za Serikali zinapaswa kuwa mfano kwa kutii sheria za nchi hususani sheria ya mazingira nimeshasema mara nyingi na ninarudia hapa tena taasisi za serikali haziruhusiwi kuchafua mazingira kwa namna yoyote ile kwa mujibu wa sheria. “ alisisitiza Mpina.
Aidha Mpina ameitaka Manispaa ya Temeke kusimamia kuwa makini na zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo ya Keko na kuwachukulia hatua wananchi wote wanaotiririsha maji taka katika mifereji ya maji ya mvua.



Akitoa ufafanuzi wa adhabu hiyo mwanasheria wa Baraza la mazingira, Suguta  Heche, amesema kuwa Tasisi za serikali na mashirika ya umma yana wajibu wa kufuata sheria za nchi hususani sheria za mazingira na ukiukwaji wa sheria hizo utaambatana na adhabu kama zinatolewa kwa mashirika na makampuni binafsi.
Awali Naibu Waziri Mpina alitembelea kiwanda cha kutengeneza dawa cha Keko Pharmaceutical limited na kutoridhishwa na uharibifu wa mazingira unaofanywa na kiwanda hicho wa kutiririsha maji taka katika makazi bila kutibiwa, na kutokuwa na kibali cha utiririshaji kutoka kwa bonde na kuwatoza faini ya shilingi milioni ishirini inayopaswa kulipwa ndani ya wiki mbili, na kuelekeza usafi wa mazingira kufanyika katika mifereji ya maji ya mvua na kuwaasa wakazi wa maeneo jirani kutokutupa takataka katika maeneo hayo.
Kwa upande wake Bwana Selemani Ndugwana, Meneja uthibiti na Ubora wa kiwanda hicho cha dawa alipokea adhabu hiyo, na kusema kwamba ni kubwa sana wanaomba serikali iwapunguzie adhabu hiyo, kwa kuwa ni kosa la mara ya kwanza. Akiwakilisha wakazi wa eneo la keko mtendaji wa kata hiyo Bwana Samweli Magali alisema kero ya uchafuzi wa mazingira unaotoka kwenye kiwanda hicho cha madawa ni kubwa na ni hatarishi kwa afya za wakazi wa eneo hilo.