Na
Naamala Samson
Wajasiriamali
waundao mtandao wa maendeleo wa GO BIG yaani “GO BIG DEVELOPMENT NETWORK”
wanatarajia kukusanya zaidi ya kiasi cha shilingi milioni mia mbili na hamsini
(250) ili kuanzisha kijiji cha mfano. Kijiji hicho kinatarajiwa kuanzishwa
mwishoni mwa mwaka huu na kitahusisha shughuli mbalimbali za wajasiriamali hao.
Akichangia
katika sherehe za kutimiza mwaka mmoja wa umoja huo zilizofanyika Vikindu nje
kidogo ya jiji la Dar Es Salaam mnamo mwanzoni mwa mwaka huu, mmoja wa walezi,
Bwana Andrew Mhina aliwaambia wajasiriamali hao, “ndugu zangu, wakati ni huu
ambapo tukianzisha kijiji cha mfano cha ‘GO BIG VILLAGE’, watu tutaweza kulima
humo, kufuga, kuzalisha bidhaa kwa wingi na kwa ubora kukidhi sio tu soko la
ndani bali na la nje”. Aliongezea kwa kusema kuwa watatumia kijiji hicho
kuongeza ajira na kujenga taifa la watu kuwa wabunifu zaidi.
Mgeni rasmi, Bw.David kutoka
shirika la nyumba la taifa (NHC) kama Mkurugenzi wa kitengo cha uwekezaji
akiwahamasisha wajasiriamali wa GO BIG. Kulia ni mlezi wa
wajasiriamali hao, Bw.Andrew Mhina na Kushoto ni Bi.Nancy Msangi, makamu
mwenyekiti wa umoja huo (Picha na Naamala Samson)
Waanzilishi wa umoja wa GO BIG,
Bwana Meshack Maganga akiwa na Bwana Mwimba Philemon ambaye pia ni mweka hazina
wa umoja huo (Picha na Naamala Samson)
“Ni
lazima tuwe vijana wa mfano, tuwe wajasiriamali wa mfano sio kwa maneno bali
kwa vitendo na tuweke nia sasa ya kuanzisha kijiji hiki kitakachotusaidia sisi
na kuinua uchumi wa nchi yetu.”, alisema Bwana Meshack Maganga ambaye ni mmoja
wa waanzilishi wa umoja huo wa wajasiriamali wa GO BIG.
Umoja
huo unaundwa na watu mbalimbali takribani mia mbili na hamsini
wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji na utoaji huduma na
wanatarajia kuchangishana kila mmoja milioni moja kwa kuanzia. Na kuzitumia
milioni mia mbili na hamsini (250) kama kianzio kununua eneo kubwa katika mkoa
utakaoteuliwa na kisha kuendelea kuanzisha katika mikoa mingine.
Akiwapa
moyo wajasiriamali wengine hasa wanawake, Bi.Sarah Filikunjombe alisema, “dada
zangu na wadogo zangu hasa wa kike, msivunjike moyo mnapoona mnapoona mnapata
changamoto kwenye kulima. Mimi nimeshapata sana hasara kwenye kilimo cha
vitunguu, matikiti na hata kwenye kufuga kuku lakini sikati tamaa na ninasonga
mbele.”
Wajasiriamali
hao walitoa rai kwa serikali kuhakikisha inasaidia wajasiriamali wa ndani ili
kuwainua kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya kuendeleza ubunifu wao, kuwatengea
maeneo maalum ya kufanyia shughuli zao bila bugudha, na kuwalegezea masharti ya
kupatikana kwa mkopo kutoka taasisi mbalimbali za kifedha.
Pamoja
na hayo, wajasiriamali hao wa GO BIG wanaotoka sehemu mbalimbali nchini,
waliweza kubadilishana uzoefu na kuhamasishana katika kilimo cha miti ya mbao,
ufugaji nyuki, kilimo cha vitunguu, matikiti, ujenzi wa nyumba za gharama nafuu
na shughuli kadhaa za huduma za chakula, huduma za kiteknolojia, vinywaji na
utoaji wa mafunzo mbalimbali, na nyinginezo nyingi.
Wajasiriamali wakifuatilia mazungumzo
Sarah Filikunjombe akiongea na
wajasiriamali wenzake wa GO BIG