DK. KIGWANGALLA ATEUA ITAKAYOCHUNGUZA ATHARI ZA BONDE LA MTO KILOMBERO

*NI kamati maalum itakayochunguza athari za bonde hilo na kumpatia majibu *Akagua maeneo mbalimbali ya bonde hilo na kuhushudia athari ... thumbnail 1 summary
*NI kamati maalum itakayochunguza athari za bonde hilo na kumpatia majibu
*Akagua maeneo mbalimbali ya bonde hilo na kuhushudia athari zaidi

Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Maliasili na Utalii Dk. Hamisi Kigwangalla (MB) ameteua Kamati maalum ambayo itaishahuri Serikali namna ya nini kifanyike katika kushughulikia  athari za bonde la Kilombero lililopo Mkoani Morogoro.

Waziri Dk Kigwangalla amebainisha kuwa Kamati hiyo aliyoiteua,  ndio itamshahuri juu ya bonde hilo litasimamiwa vipi pamoja na namna bora ya hatua za kuchukua ili kulinda bonde hilo ambalo lina mahitaji makubwa ikiwemo chanzo kikubwa  cha maji yanayotengeneza Stiegler’s Gorge ambako Serikali imeamua kuweka mikakati ya utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme unaotarajiwa kufikia megawatts 2100 huku pia bonde hilo likiwa na utajiri wa kuwepo na aina zaidi ya 400 ya ndege pamoja na mnyama anaina ya Puku ama Sheshe ambaye hapatiani duniani kote zaidi ya Tanzania pekee.

"Hii ndio Kamati yangu, itakayonishahuri juu ya bonde ili litasimamiwa vipi. Hii ndio Kamati ambayo itanishahuri mimi na kwamaana hiyo Serikali kwa ujumla wake juu ya namna bora ya uhifadhi hususani katika eneo lile la Pori tengefu.

Hapa kuna vitu viwili vya kuzingatia: Ardhi Ohevu (Ramsar site) ambalo lina eneo lake huku pia eneo la pori tengefu nalo kichukua nafasi kubwa zaidi" Amesem Waziri Dk Kigwangalla wakati wa kuteua Kamati hiyo.

Kamati hiyo inaundwa na  wajumbe mbalimbali ambao wataongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Ndugu Andrew Napacho, Pia wajumbe ni  Brig. Gen. (Mst.) Edmund Mndolwa, Aliyekuwa Kamanda wa Polisi katika Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Mstaafu, Suleiman Kova, Mwenyekiti Taifa wa Chama Cha wafugaji Bwana  Semkae Kilonzo (Policy Forum).

Wengine ni  Dk. Simon Mduma, Prof. Jaffar Kideghesho, Ruzika Muheto, Mkuu wa Wilaya ya Ulanga, MKuu wa Wilaya ya Kilombero na Mkuu wa Wilaya ya Malinyi.

Wemgine ni Mwenyekiti Halmashauri Ulanga, M/Halmashauri Kilombero, M/Halmashauri Malinyi  na M/Halmashauri Ifakara.

Pia yupo  Mtendaji Mkuu wa KPL, Mtendaji MKuu wa Illovo, Mkuu Kikosi JKT Chita. Wengine ni  Dk. Aggrey Mlimuka, Mwakilishi kutoka mamlaka ya maji Bonde la Kilombero, Mwakilishi kutoka Wizara ya ardhi.

Wajumbe wengine ni Ndugu.  Innocent Kylogeris, Dk. James Wakibara pamoja na Mkurugenzi Mkuu TAWA ambaye atakuwa Katibu wa Kamati hiyo.

Hatua hiyo inafuatia Waziri Dk Kigwangalla kufanya ziara maalum kwenye bonde hilo la kilombero ambapo ameweza kushuhudia athari kubwa zaidi zilizofanywa na wavamizi wakiwemo wakulima na wafugaji ambao wameonekana kuvamia maeneo makubwa  ndani ya pori tengefu la bonde pamoja na Kwenye eneo ohevu ndani ya bonde hilo.