BIOGESI KUPUNGUZA MATUMIZI YA KUNI NCHINI

Mwandishi wetu, Dodoma TAKRIBANI tani 3 za kuni zinazotumika kwa kila kaya kwa mwaka hazitatumika tena kufuatia Programu ya uendelezaji B... thumbnail 1 summary
Mwandishi wetu, Dodoma
TAKRIBANI tani 3 za kuni zinazotumika kwa kila kaya kwa mwaka hazitatumika tena kufuatia Programu ya uendelezaji Biogesi TanzaniaTDBP kufunga mitambo ya biogesi katika kaya 4500 katika Mikoa 11 nchini.
Mikoa ambayo itanufaika na mpango huo katika hatua za awali ni pamoja ni Kilimanjaro, Arusha, Tanga, Pwani, Manyara, Dar-es-salaam, Dodoma, Singida, Mbeya, Iringa na Njombe.
Hayo yamebainishwa na mratibu wa TDPB lehada Shilla mjini Dodoma katika Mkutano wa kupanga rasimu ya utekelezaji wa mwaka 2013 uliofanyika Mjini Dodoma kwa lengo la kuboresha matumizi ya biogesi na hivyo kupunguza uharibifu wa mazingira.
Wadau wa uendelezaji wa Biogesi kutoka mikoa mbalimbali wameelezea changamoto wanazokutana nazo ikiwemo uwezo mdogo wa wananchi kuweza kufungiwa mitambo hiyo.
Mwaka 2013 TDBP imelenga kufunga mitambo ya Biogesi ipatayo 3300 katika maeneo mbalimbali Nchini hatua itakayosaidia kukuza uchumi na kuondokana na ukataji miti ovyo unaochangia athari hasi za tabia nchi.