Umoja wa mataifa unasema kilimo cha bangi nchini Burma kimeongezeka kwa mwaka wa sita mtawalia.
Inasemekana wakulima hawakuwa na mazao mbadala ya kukuza kando na bangi hiyo ambayo hutumika kama kilewesha kwa kuwa ni zao lenye faida kubwa kifedha.
Burma ni nchi ya pili duniani inayokuza kwa wingi bangi baada ya Afghanistan.
Mwandishi wa BBC anasema hakuna jitihada kamili za kumaliza ukuwaji wa bangi kwa kuwa jeshi nchini humo na makundi ya wanamgambo yananufaika kutokana na biashara hiyo.
Chanzo: BBC