KWANINI PAMBANA NA CLIMATE CHANGE?

Malengo ya Pambana na Climate Change ni kukupatia taarifa mbalimbali za mabadiliko ya tabia nchi, mazingira, maliasili na utalii. Lengo ni ... thumbnail 1 summary
Malengo ya Pambana na Climate Change ni kukupatia taarifa mbalimbali za mabadiliko ya tabia nchi, mazingira, maliasili na utalii. Lengo ni kukupatia taarifa sahihi juu ya sababu, madhara ya mabadiliko ya tabia nchi na hatua muhimu ambazo unatakiwa kuzichukua kukabilina nayo.
Tusichukulie kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni jambo lisilotuhusu na kwamba linatupotezea muda, la hasha, mabadiliko ya tabia nchi yanamadhara makubwa sana katika jamii yote. Na tayari madhara makubwa yameshatokea na kusababisha vifo vya watu wengi na athari nyingine.



Kwa kuorodhesha madhara machache yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi ni pamoja na ukame, njaa, mafuriko, tetemeko la ardhi na kuongezeka kwa joto duniani, magonjwa na kadhalika.
Hali hii inatutaka sisi wote kusimama imara kushika silaha na kuanza kupamba na vita hii ambayo haingoji kesho bali leo, hali hii ya joto duniani sio ya kawaida, kizazi kijacho kitaungua na kushindwa kuishi.
Kupitia blog hii utajifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, pia utapata habari mbalimbali za mabadiliko ya tabia nchi na mazingira, na kutoa ufafanuzi wa misamiati migumu ya mazingira ili uweze kupata uelewa wa kutosha juu ya jambo hili.
Pia blog hii itakupatia njia mbadala za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa kutumia nishati mbadala na njia nyinginezo ambazo ni rafiki wa mzingira, muda wa kuandaa mikakati, kujipanga, kuandaa utaratibu umepitwa na wakati na sasa ni muda wa kutenda, tutende kwa pamoja tutashinda.