Jamii ya watu wanaozungukwa na Mlima
Balili uliopo wilaya ya Bunda mkoani Mara wamefaidika na Mradi wa
kuwajengea uwezo kuhusu kutunza Mlima
huo ulioandaliwa na Asasi Lubana
Corridor Environmental Development Strategy ya wilayani humo uliofadhili wa na Taasisi ya The
Foundation for Civil Society ya jijini Dar es Salaama kwa mwaka 2009/2010.
Mratibu
wa Asasi hiyo Bw Daudi Masalu alisema kuwa
Mradi uliokuwa na thamaini ya shilingi zaidi 34 ulikuwa ukivihusu vijiji
12
vilivyokuwa vinazunguka Mlima huo ambavyo ni pamoja na vijiji vya
Balili,Bukole,Nyamakoto,yamatoke,Kunzugu,Mihale,Changuge,Mchalo,Ligamba
A,Ligamba B,Chilinge na Saragana.
Alisema kukamilika kwa Mradi huo kumeleta faida
kubwa katika Asasi hiyo ikiwa ni pamoja
na wanaasasi kupata Mafunzo ya namna ya kusimamia Miradi,kubuni Miradi na
kutekeleza Miradi kwa ufanisi mkubwa.
“Kwa kweli
tumenyfaika sana na huu Mradi tuliofadhiliwa na hawa Foundation for Civil
Society maana tusingeweza kama wasingekubali kutuwezesha” alisema Bw Masalu
Bw. Masalu alisema kuwa katika kutekeleza Mradi huo
Jamii imeonyesha Mabadiliko makubwa ambao kwa pamoja waliamua kuunda Vikundi
mbalimbali vya kupanda miti katika Mlima huo,kufuga Nyuki,kubuni Majiko Banifu
ambayo yalikuwa mbadala baadala ya kutumia Kuni na kuendelea kuharibu Mazingira
ya Mlima huo.
Alisema baaada ya kuendesha Mradi huo kwa Mafanikio
makubwa wananchi hao wanaozungukwa na Mlima huo waliamua kuunda sheria ndogo
ambazo zilikuwa na lengo la kuulinda Mlima huo usiharibiwe na wananchi
waliokuwa wamezoe kufanya vitendo vya kuharibu Mazingira.
“Baada ya
kuutekeleza Mradi huu wananchi walipata ufahamu wa kutosha na kuamua kuunda
vikundi mbalimbali vya kuulinda Mlima Balili na kutunga sheria ndogo katika
maeneo yao” alisema Mratibu huyo.
Katika kuutekeleza Mradi huo Mratibu huyo alisema
kuwa waliweza kushirikisha Makundi mbalimbali ambaayo waliona yana umuhimu wa
kufnya hivyo kama vile Walemavu ambao nao waliamua kuanzisha kikundi chao cha
kupambana na Umaskini kwa kufanya shughuli ndogondogo kama Ufundi Seremala na
hiyo ni baada ya kupata Mafunzo kutoka Asasi hiyo ya Lubana.
Pamoja na kushirikisha baadhi ya Makundi katika
Jamii,Bw Masalu aalisema kuwa Jamii
ilishirkishwa kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha Mradi huo kama vile kutunza
vyanzo vya Maji,upandaji miti,matumizi mazuri ya kuni na kutunza Mazingira ya
Mlima huo.
Mbali na hivyo pia Jamii ilishirikishwa katika
kubuni MiradiKupanga Miradi huku baada ya sekta na viongozi wa vijiji huska
wakialikwa katika semina mbalimbali kujengewa uwezo wa kutunza Mazingira hasa
yaa Mlima Balili.
“
Tumejitahidi sana kushirikisha baadhi ya sekta na viongozi wa Vijiji katika
kuwapatia semina na Mafunzo mbalimbali katika utunzaji wa Mazingira na hasa
Mlima Balili” alisema Mratibu huyo.
Kuhusu Mahusiano yalipo kati ya Asasi hiyo na
Wafadhili wengine tofauti na The Foundatio for Civil Society,mratibu huyo
alisema kuwa Mahusiano ni mazuri kuanzia katika Halmashauri ya wilaya ya Bunda
na baaadhi ya Taasisi zingine kutoka nje ya nchi.
Alisema mahusiano hayo kuwa Mazuri yanatokana na
Asasi yao kujitoa katika kusaidia mambo mbalimbali yanayoizunguka Jamii na
hivyo wanajamii kuona umuhimu wa Asasi hiyo huku akitolea mfano Halmashauri
kuwaletea baadhi ya Miradi kutoka kwa wafadhili wa nje wanaotaka kusrikiana na
Asasi ya wilayani hapoanikisha.
Katika kufanikisha Jambo lolote Mratibu huyo alisema
kuwa haliwezi kukosa Changamoto huku akieleza kuwa kumekuwepo na changamoto
kubwa katika kukamilisha Mradi huo ambao mwishoni ulionekana kuleta Mafanikio
makubwa kwa wananchi wa Vijiji hivyo 12.
Bw Masalu alisema kuwa changamoto kubwa ilikuwa ni
kuwafikia Walengwa kutokana na Jiografia ya eneo hilo la Mlima,wananchi
kutokuwae na elimu ya kutosha katika kutunza Mazingira,baadhi ya watu walikuwa
wakiishi kwa kutegemea Mlima huo kama chanzo chao cha kujipatia Kipato na
Maporomo yaliyokuwa yakitokea katika Mlima huo wakati wa kutekeleza Mradi huo.
‘Ndugu yangu
kitu chochote hakikosi Changamoto na
katika mradi huu changamoto ilikuwa kubwa kutokana na Jiografia ya Mlim huo
yaani ilikuwa tabu sana “ alisema Bw Masalu
Wakiongelea faida walizozipata kutokana na
kutekelezwa kwa Mradi huo Bi Mary Mpanda mkazi wa kijiji cha Kunzugu alisemaa
kuwa alipata faida kubwa kutokana na
kujua umuhimu wa kutunza Mazingira,kutumia Majiko banifu kwa kuamini kuwa
kutumia kuni ni kuendelea kuharibu Mazingira.
‘Kiukweli
nilipata faida kubwa sana hasa katika suala la kutunza Mazingira na kutumia
Majiko Banifu kwani niliona kuendelea kutumia kuni ni kuharibu Mazingira”
Alisema Bi Mary
Naye Bi Dotto Bukangi alisema kuwa alinufaika katika
suala la kutunza Mazingira,kuziba Makongoro na kutumia Majiko banifu na kufikia
Majirani kuona kuwa kuna umuhimu wa kutunza Mazingira.
Aidha akiongelea kuhusu Mradi huo Bi Lidia Mogasa
ambaye ni Bi shamba kutoka Halmshauri ya wilaya ya Bunda alisema kuwa Mradi huo
umeleta manufaa makubwa kwa Jamii kutokana na Mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na
Asasi hiyo ambapo Jamii imeonekana kubadilika kwa asilimia kubwa.
“Ni kweli
mradi huo ulitusaidia sana maana Mafunzo tulipata mengi sana na mabadiliko
yameonekana katika Jamii yetu katika kutunza Mazingira” alisema Bi Lidia
Katika kuonyesha kufaidika na ruzuku hiyo ya Taasisi
ya The Foundation for Civil Society,Bw Masalu alisema kuwa Taasisi hiyo
imewasaidia katika kuwajengea uwezo wa kusimamia Mradi,kusimamia
fedha,kuhudulia Semina mbalimbali,kuhudhulia katika Maonyesho ya AZAKI mara
tatu mfululizo.
Pia Taasisi ya The Foundation for Civil Society
imetusaidia kupata vifaa vifaa vya Ofisi huku Jamii ikionekana kuiamini Asasi
hiyo kutokana na kuaminika na baadhi ya Taasisi kubwa kama The Foundation for
Civil Society.
Chanzo: mwanawaafrika blog