Masoud Masasi,Dodoma
JUMLA
ya washiriki 16 kati ya 36 wamepatikana katika mchujo wa kuwapata
washiriki watakaoshiriki katika mashindano ya kumtafuta mrembo wa utali
kwa mkoa wa Dodoma inayotarajiwa kufanyika Novemba 9 mwaka huu mjini
hapa.
Mkurugenzi
wa Island Promotion Tanzania ambao ndio waratibu wa shindano hilo
Nyanza Lydenge alisema katika mchujo huo washiriki 16 walipatikana
ambao wataanza mazoezi octoba 13 mwaka huu ambapo amesema watafanya
mazoezi kwa kipindi cha wiki tatu kabla ya kuingia rasmi kambini.
Lydenge
aliwataja washiriki hao waliopita katika mchujo huo kuwa ni Rachel
Kilongo,Jamila Said,Pulcheria Paul,Amina Ayoub,Tibaijuka
Leornad,Lightness Kitua,Bertha Patrick,Furaha Kinyunyu,Johan John,Erika
Elibariki,Sarafina Jackson,Happy Elias,Sabra Habibu,May Singano,Jesca
Peter na Naima Habibu.
“Hawa
washiriki 16 tumewapitisha baada ya kuzingatia vigezo vyao
tumeridhishwa nao lakini wakati wanafanya mazoezi tutawaangalia pia kwa
wale ambao watakuwa na nidhamu mbovu tutawapunguza kwani tunataka
mshindi mwenye nidhamu ya hali ya juu”alisema Lydenge.
Alisema
washiriki hao katika kipindi hicho watapata fursa ya kutembelea vivutio
mbalimbali vya mkoa wa Dodoma katika kuweza kuvitangaza ili viweze
kutambuliwa na wadau nchini.
“Wakati
wa mazoezi tutawapeleka washiriki kwenda kutangaza vivutio vya utalii
mkoa wa Dodoma ambavyo viko sehemu mbalimbali lakini sisi tutakwenda
wilayani kondoa lengo ni kuvitangaza vivutio hivyo mkoani hapa ”alisema
mkurugenzi huyo.
Chanzo: Dodoma Yetu