Inakadiriwa kuwa watu zaidi ya 200
huuawa na wanyama pori kwa mwaka Tanzania, wanyama hao hatari ni simba, mamba, tembo,
viboko, fisi na nyoka na kwamba idadi hiyo ya watu kupoteza maisha inaweza kuwa
mara mbili ya idadi hiyo huku simba wakitajwa kufanya mauaji hayo kwa asilimia
70.
Mtafiti wa mambo ya wanyama Craig
Packer ameeleza kuwa kati ya mwaka 1990 hadi 2004 watu 815 walivamiwa na simba
na 563 kuuawa nchini Tanzania.
Wanasayansi kutoka America na
Tanzania pia wanaripoti kuwa hali ya binadamu kuliwa na wanyama pori hasa katika
maeneo ya vijijini yameongezeka kwa kasi katika kipindi cha mwaka 1990 hadi
2005 ambapo katika kipindi hicho wakazi zaidi ya 500 walipoteza maisha yao kwa
kuliwa na simba na kuuawa na wanyama kama tembo.
Idadi hiyo inaonekana kuwa kubwa na
kufananishwa na ya karne iliyopita ambapo matukio kama hayo yalijitokeza zaidi
katika msitu wa Tsavo.
Matukio hayo yamejitokeza zaidi katika hifadhi ya Selous katika wilaya ya Rufiji, Lindi na maeneo ya
mipakani mwa Msumbiji na Tanzania
Pamoja na sababu kubwa ya mauaji hayo kusababishwa na wananchi
kuweka makazi katika maeneo ya hifadhi na kufanya shughuli za kila siku katika
hifadhi za taifa, lakini wataalamu wanasema kuwa sera za uhifadhi wa mazingira
na hifadhi za taifa zinapaswa kutumika ili kupunguza tatizo hili.
Tabianchi