Waziri
wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk wamwanzo kulia
akimpa zawadi Balozi wa Uingereza Nchini Tanzania Diane Conr ner Baada
ya kufanya Mazungumzo kuhusiana na mambo mbalimbali ya Michezo na
maendeleo ya Digital hapo Afisini kwake Kikwajuni Zanzibar.
Waziri
wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk wamwanzo kulia
akipeana mikono na Balozi wa Uingereza Nchini Tanzania Diane Conr ner
Baada ya kufanya Mazungumzo kuhusiana na mambo mbalimbali
ya Michezo na maendeleo ya Digital hapo Afisini kwake Kikwajuni Zanzibar.
ya Michezo na maendeleo ya Digital hapo Afisini kwake Kikwajuni Zanzibar.
Waziri
wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk wamwanzo kulia
akifanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza Nchini Tanzania Diane Conr
ner kuhusiana na mambo mbalimbali ya Michezo na maendeleo ya Digital
hapo Afisini kwake Kikwajuni Zanzibar.
Baadhi
ya Watendaji wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo
wakimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Diane Conr ner(hayupo
pichani) alipokutana na Waziri wa Habari wa Zanzibar hapo Afisini kwake
Kikwajuni.Picha na Yussuf Simai, Maelezo
-------------------------------------------
YUSSUF SIMAI.MAELEZO ZANZIBAR
Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema kuwa Zanzibar itahakikisha inaingia
katika Mfumo wa Digital kabla ya kufikia tarehe iliowekwa ili kwenda sambamba na mabadiliko ya Ulimwengu. Waziri ameyasema hayo hapo Afisinikwake Kikwajuni wakati alipofanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Diane Conrner .
-------------------------------------------
YUSSUF SIMAI.MAELEZO ZANZIBAR
Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk amesema kuwa Zanzibar itahakikisha inaingia
katika Mfumo wa Digital kabla ya kufikia tarehe iliowekwa ili kwenda sambamba na mabadiliko ya Ulimwengu. Waziri ameyasema hayo hapo Afisinikwake Kikwajuni wakati alipofanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Diane Conrner .
Amesema
licha ya Zanzibar kuingia katika Mfumo wa Digital lakini inakabiliwa na
changamoto nyingi ikiwa pamoja na Vifaa na mafunzo kwa watendaji wake.
Akizungumzia Sekta ya Utalii Waziri Mbarouk alisema kuwa sekta hio
inakua kwa kasi kubwa kutokana na Wawekezaji Binafsi ambao huwekeza
Zanzibar na kuweza kuitangaza zaidi katika miji na Nchi tafauti.
Aidha
amesema kuwa Serikali inafarijika kuona Watalii wengi kutoka Uingereza
na nchi nyengine za Ulaya wanafika Zanzibar na kutembelea sehemu
mbalimbali za kihistiria
na vivutio vyengine vya Utalii vilivyopo nchini.
na vivutio vyengine vya Utalii vilivyopo nchini.
Nae
Balozi huyo Diane Conrner ameipongeza Zanzibar kwa juhudi kubwa
inazochukua katika kuimarisha sekta ya utalii na kueleza matumaini yake
kuwa sekta hiyo itaendelea kuwa muhimili mkubwa wa uchumi.
Akizungumzia
sekta ya michezo Balozi Diane ameishauri Serikali ya Mapinduzi ya
ZanzĂbar kushiriki michezo mbali mbali ikiwemo ya Kimataifa kwa vile
michezo inatoa mchango mkubwa katika kuitanga nchi kujulikana duniani
kote.
Akitoa mfano wa
Michezo ya Olimpiki iliofanyika mjini London, Uingereza, mwaka huu amesema
imeweza kuipatia sifa kubwa Nchi yake pamoja na Faida mbalimbali za kiuchumi na
kijamii.
Waziri Saidi
amemshukuru Balozi huyo kwa Kufika kwake Zanzibar na kuweza kuzungumza na
viongozi masuala mbalimbali yenye umuhimu kwa nchi
na jamii kwa jumla.