na Berensi Alikadi, Bunda
IDARA ya Uvuvi
wilayani Bunda, Mara imefanikiwa kukamata zana mbalimbali haramu za uvuvi
zipatazo 660 zenye thamani ya sh milioni 15.
Akizungumza na
waandishi wa habari jana ofisini kwake, Ofisa Uvuvi wa wilaya hiyo, Steven
Ochien’g, alisema zana hizo zilikamatwa kati ya Julai na Desemba mwaka jana.
Alisema katika
msako huo walioufanya katika vijiji vya Guta, Mwisenyi, Mayoro, Nyamitwebili,
Kibara, Kisorya na katika Kisiwa cha Nafuba walikamata zana mbalimbali ambazo
haziruhusiwi kuvua.
Alizitaja zana
zilizokamatwa kuwa ni makokoro ya sangara 45, makokoro ya dagaa 15, nyavu za
timba 20 na nyavu zenye matundu madogo 600 na kwamba mwaka huu wamefanikiwa
kukamata makokoro ya sangara 10 yenye thamani ya sh milioni 15.
Alibainisha
kuwa katika zoezi hilo watuhumiwa watano walikamatwa na kwamba kesi tatu zipo
mahakamani na nyingine upelelezi unaendelea.
Chanzo:
Tanzania Daima