ZANA HARAMU 660 ZAKAMATWA

na Berensi Alikadi, Bunda IDARA ya Uvuvi wilayani Bunda, Mara imefanikiwa kukamata zana mbalimbali haramu za uvuvi zipatazo 660 zenye tha... thumbnail 1 summary
na Berensi Alikadi, Bunda
IDARA ya Uvuvi wilayani Bunda, Mara imefanikiwa kukamata zana mbalimbali haramu za uvuvi zipatazo 660 zenye thamani ya sh milioni 15.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Ofisa Uvuvi wa wilaya hiyo, Steven Ochien’g, alisema zana hizo zilikamatwa kati ya Julai na Desemba mwaka jana.
Alisema katika msako huo walioufanya katika vijiji vya Guta, Mwisenyi, Mayoro, Nyamitwebili, Kibara, Kisorya na katika Kisiwa cha Nafuba walikamata zana mbalimbali ambazo haziruhusiwi kuvua.
Alizitaja zana zilizokamatwa kuwa ni makokoro ya sangara 45, makokoro ya dagaa 15, nyavu za timba 20 na nyavu zenye matundu madogo 600 na kwamba mwaka huu wamefanikiwa kukamata makokoro ya sangara 10 yenye thamani ya sh milioni 15.
Alibainisha kuwa katika zoezi hilo watuhumiwa watano walikamatwa na kwamba kesi tatu zipo mahakamani na nyingine upelelezi unaendelea.
Chanzo: Tanzania Daima