Akizungumza na NIPASHE jijini Dar es Salaam, Wigenge alisema sampuli nyingi za mbogamboga pamoja na vyakula ambavyo havifungashwi, zimechukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabala na zingine zimepelekwa Ulaya kwa uchunguzi zaidi.
Alisema uchunguzi huo unahusisha maeneo yote yanayohusu vyakula visivyo fungashwa na baadhi ya dawa zinazotokana na mabaki ya mifugo ili kubaini kama zina madhara kiafya kwa watumiaji.
Aidha, Wigenge, alisema kuwa majibu ya vipimo vya sampuli hizo yatatolewa Desemba mwaka huu, baada ya kumaliza ukusanyaji na upitiaji wa majibu hayo kutoka maabara ya ndani na nje ya nchi ili kubaini mabaki ya vimelea na madhara yake
CHANZO:
NIPASHE