Tyler Amstrong
mtoto wa miaka 8 amejikuta akipenda kupanda milima mbalimbali ulimwenguni
kutokana na kuvutika na jambo hilo alilolianza akiwa na umri wa mika saba.
Akiwa na miaka
saba alipanda mlima Whitney na kumfanya kuwa mpanda mlima mdogo kuwahi kupanda
mlima huo ulioko Calfonia Marekani kwa siku moja.
Mwezi wa saba
mwaka huu alipanda mlima Kilimanjaro ambapo wasaidizi na wabeba mizigo ya
wapanda mlima walilazimika kumwimbia nyimbo mbalimbali kama pongezi kwake.