Nimepokea
maoni tofauti tofauti kutoka kwa wadau wa mambo ya usafiri wa anga wakionyesha
masikitiko yao kutokana na kusogezwa mbele kwa safari ya kwanza ya kimataifa ya
ndege ya fastjet kutoka Dar es Salaam kwenda Johannesburg wengi wakiwa na
wasiwasi huenda shirika hilo linafanyiwa hujuma ili kulipunguza kasi yake ya
kutoa huduma bora kwa bei nafuu.
Watu
wamesikitika kwa sababu waliipania safari hii ambayo nauli yake ni shilingi
160,000 tu kwa safari moja lakini Kuna neno moja babu yangu alipenda sana
kulitumia enzi za uhai wake "Kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa
maongezi".
Kama
hujui mimi mwenyewe nilikuwa miongoni mwa waliotakiwa kufunga mkanda kwenda
Bondeni kuwaona jamaa zangu lakini kuahirishwa kwa uzinduzi wa safari hii
hakukatishi ndoto yangu hiyo.
Nakumbuka
namna jamii ilivyoipokea kwa furaha habari ya fastjet kuanzisha safari za
kimataifa kwa bei nafuu ambayo itawezesha maelfu ya wasafiri wa kada mbalimbali
kufanya safari zao mara tatu kwa wiki kwenda bondeni na kurudi Tanzania.
Pamoja
na fastjet kujipanga vya kutosha na kuonyesha ukomavu katika kutoa huduma za
usafiri wa ndege imejikuta katika wakati mgumu baada ya kulazimika kusogeza
mbele safari hiyo ambayo ilipangwa kuanza Septemba 27 mwaka huu kutokana na
sababu zilizo nje ya uwezo wao.
Katika
taarifa yao fastjet wamesema “Uzinduzi wa s
Fastjet
wameomba radhi kwa wateja wake kwa usumbufu uliojitokeza, wamesema WE ARE SORY,
nikamsikia na kasuka amerudia maneno hayohayo. Jamani kuna watu wengine kusema
samahani wagumu balaa, na kuna wengie kusamehe wenzao ni kazi kwelikweli lakini
niseme tu SAMAHANI ni kauli ya kiungwana ambayo inaonyesha kutambua makosa na
kuomba radhi ili mambo yaendelee mbele kama kawaida.
Mimi
nimeshawasamehe, nakuomba na wewe ufanye hivyo ili tusonge mbele
By
the way fastjet wameahidi kurejesha nauli kwa wateja wote walioathirika na
kadhia hiyo "W