Jiji Dar mwenyeji mkutano wa mabadiliko ya tabianchi

HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Baraza la Afrika kuhusu ufumbuzi wa mabadiliko ya ... thumbnail 1 summary
HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa kimataifa wa Baraza la Afrika kuhusu ufumbuzi wa mabadiliko ya tabianchi, utakaofanyika Oktoba 30, mwaka huu hadi Novemba mosi.

Akizungumzia jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meya wa jiji hilo, Dk. Didas Masaburi, alisema mkutano huo unaojulikana kwa jina la ‘International Local Government for Sustainability’ utashirikisha pia Jumuiya ya Tawala za Mitaa, ‘ALAT’.

Alisema kuwa mkutano huo utalenga kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika ngazi ya serikali ya mtaa ambayo yanakumbana na changamoto mbalimbali ikiwamo mabadiliko ya hali ya nchi.

“Nawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi ili wajue athari za kukaa kwenye maeneo mabaya, kujenga miji thabiti na stahimilivu kwa maendeleo na ustawi wa nchi yetu,” alisema.

Dk. Masaburi aliomba mashirika mbalimbali ya ndani ya nchi na nje ya nchi kujitokeza kusimamia mkutano huo il ikutoa fursa kwa wao kujitangaza kibiashara.

Chanzo: Mtanzania