KIKOSI CHA KUDHIBITI UJANGILI CHAENDA KUSAKA FISI WANAOKULA WATOTO GEITA

KIKOSI dhidi ya ujangili kanda ya ziwa(KDU),kimelazimika kwenda katika kijiji cha Nyamboge tarafa ya Bugando wilayani Geita kuwasaka Fisi w... thumbnail 1 summary
KIKOSI dhidi ya ujangili kanda ya ziwa(KDU),kimelazimika kwenda katika kijiji cha Nyamboge tarafa ya Bugando wilayani Geita kuwasaka Fisi wanaodaiwa kuwa tishio kwa maisha ya binadamu hasa watoto.
Kiongozi wa kikosi hicho ambaye ni Ofisa wanyama pori wilaya ya Nyang’hwale,Samweli Mwita,amesema kikosi hicho cha Kuthibiti Ujangili kitakuwa na watu wane wawili kutoka Mwanza na wengine kutoka wilaya za Geita na Nyang’hwale.

Amesema hatua hiyo imekuja kufuatia tukio la mtoto,Joshua Pambano(3)mkazi wa Nyamboge kupoteza maisha kwa kushambuli na kuliwa na fisi.

Mtoto huyo alinyakuliwa na fisi juzi akiwa Nyumbani kwao majira ya saa 1:30 usiku na juhudi za wananchi kumpata akiwa hai hazikuzaa matunda baada ya kukuta ametafunwa na kubaki vipande vidogo vya fuvu la kichwa.

Tukio hilo ni la pili kutokea kijijini hapo katika kipindi kisichozidi miezi minne ambapo mwezi wa tano Mwaka huu mtoto Stephano Madeni(2)aliuawa kwa kuliwa na fisi.


Wanyama hao wanadaiwa kutapakaa katika makazi ya watu kutokana na Uharibifu wa mazingira ya Mistu ambapo wamekuwa wakihama kutoka porini kwa kukosa chakula na kwenda kwenye makazi ya watu.