Kuharibiwa kwa tabaka la ozone chanzo cha upofu na mtoto wa jicho

Mkurugenzi idara ya mazingira ofisi yamakamu wa Rais Dkt Julius Ningu akisoma hotuba ya ufunguzi katika maadhimisho ya siku ya kimaifa ya... thumbnail 1 summary
Mkurugenzi idara ya mazingira ofisi yamakamu wa Rais Dkt Julius Ningu akisoma hotuba ya ufunguzi katika maadhimisho ya siku ya kimaifa ya hifadhi ya tabaka la ozone inayofanyika kitaifa mjini mwanza leo.

Na Evelyn Mkokoi

Imelezwa kuwa kuharibiwa kwa tabaka la ozoni husababisha kuongezeka kwa magonjwa, kama vile saratani ya ngozi, uharibifu wa macho kama vile "mtoto wa jicho" unaosababisha upofu, na upungufu wa uwezo wa mwili kujikinga na maradhi.
hayo yameelezwa leo Jijini Mwanza  na mkurugenzi wa idara ya mazingira kutoka ofisi ya makamu wa rais Dkt Julius Ningu katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya hifadhi ya tabaka la ozoni.
Picha ya pamoja ya washiriki wa warsha katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya hifadhi ya tabaka la ozone inayofanyika kitaifa mjini mwanza leo.picha na habari na (Evelyn Mkokoi)

Dkt. Ningu amesema kuwa  watoto wako katika hatari zaidi ya kupata madhara haya, na madhara mengine  katika viumbe hai, pamoja na  kuharibika kwa fiziolojia ya mimea na utaratibu wa ukuaji wake.

Dkt Ningu ameendelea kusema kuwa, madhara haya yanaweza kuchangia mabadiliko katika muundo wa spishi, hivyo kuathiri  bioanuwai katika mifumo ikolojia mbalimbali, na yaweza kuchangia kuathiri uzalishaji, ukuaji na uwezo wa kuzaliana wa viumbe wa majini,  na uharibifu wa vifaa mbalimbali vya aina ya plastiki.

Awali akifungua mafunzo kwa washiriki ikiwa ni sehemu ya kazi katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya hifadhi ya tabaka la ozoni, Mgurugenzi msaidizi osifi ya kamau wa rais mazingira bi Magdalena Mtengu amesema kuwa kumong’onyoka kwa  tabaka hilo kutokana na mlundikano wa gesi aina mbali mbali.

alitolea mfano wa gesi hizo kuwa  kuwa  ni pamoja na, chloroflourocarbons (CFCs), halons, methyl choroform, methyl bromide, carbon tertrachoridena ambazo ni sehemu ya kemikali zinazotumika katika majokofu, viyoyozi, vifaa vya kuzimia moto, ushafishaji chuma, utengenezaji wa magodoro, madawa na manukato ya kupulizia, ufukizaji wa udongo katika vitalu vya tumbaku na mashamba ya maua na upiliziaji wa madawa kwenye mazao katika maghala.

Na  Ili kunusuru uharibifu wa tabaka la ozone na madhara yake kwa viumbe hai na mimea serikali za jumuiya ya umoja wa kimataifa kwa pamoja ziliridhia Mikataba mbali mbali ukiwemo wa Montreal wenye lengo la  kudhibiti utengenezaji na matumizi ya kemikali zinazomong’onyoa Tabaka hilo.


maadhimisho haya kitaifa mwaka huu yanafanyika mjini mwanza yakiwa na malengo ya kutoa mafunzo kwa mafundi, wenye viwanda na elimu kwa wananchi kupitia vyombo vya habari.