Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais Muungano kushoto mh. Samia suluhu Hassan kwa Niaba ya waziri wa
nchi wa nchi Ofisi ya makamu wa Rais Mazingira Dkt Terezya Hufisa, akisoma
hotuba kwa waandishi wa habari hawapo pichani kuelekea maadhimisho ya siku ya kimataifa
ya hifadhi ya tabaka la Ozone, ambayo huadhimishwa kila mwaka Sepetember 16
kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt Julius
Ningu (Picha na Ofisia ya Makamu wa Rais)
Na Evelyn Mkokoi & Rashda Rashid
Ili kufanikisha utekelezaji wa mkataba wa Montreal, serikali
imeandaa na kutekeleza programu ya Taifa ya kuondosha matumizi ya kemikali
haribifu kwa tabaka la ozoni.
Akiongea kwa Niaba ya ya waziri wanchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Mazingira waziri mwenye dhamana ya kushughulikia masuala ya Muungano Mh.
Samia Hassan Suluhu alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo,
amesema mikakati ya kitaifa ndani ya Programu hii ni pamoja na kujenga uwezo wa
taasisi zinazosimamia utekelezaji wa mkataba, kutoa elimu kwa wadau na umma wa
watanzania kuhusu umuhimu wa Tabaka la Ozoni na hatari zinazolikabili.
Mheshimiwa suluhu aliongeza kwa kusema kuwa kubadilisha
technolojia katika viwanda vinavyotumia kemikali haribifu na kutoa mafunzo
yanayolenga kuimarisha ujuzi katika sekta ya kuhudumia viyoyozi na majokofu na kuhamasisha na
kuhimiza matumizi ya kemikali na technolojia mbadala na rafiki kwa tabaka la
Ozoni ni njia ambazo serikali inatumia kunusuru kuharibika kwa tabaka la hewa
ya Ozoni
“Ni muhimu tuzingatie
kwamba juhudi za kila mmoja wetu zinatakiwa kupunguza na kuondosha mathara
katika Tabaka la Ozoni yanayo sababishwa na bidhaa tunazo nunua na kutumia
majumbani au sehemu za biashara alisisitiza.”
Mh Suluhu aliwaasa wananchi kushiriki katika kuhifadhi
Tabaka la Ozoni kwa kuzingatia kuepuka
kuingiza nchini gesi zilizopigwa marufuku, kuepuka kutupa ovyo majokofu na
viyoyozi chakavu ama vifaa vya kuzuia moto vyenye kemikali zinazomong’onyoa
tabaka la Ozoni,
Alitoa wito kwa mafundi wa majokofu na viyoyozi waakikishe
kuwa wananasa kwa kutumia tena vipoozi
(refrigerants) kutoka kwenye viyoyozi, na majokofu wanayo hudumia badala
ya kuviachia huru ili visisambae angani na amewashauri mafundi hao watoe elimu
kwa wateja wao juu ya njia raisi za kutambua uvujaji wa vipoozi.
Maadhimisho hayo ya siku ya Ozoni duniani ambayo huadhimishwa
tarehe 19 ya mwezi wa September kila mwaka, mwaka huu yatafanyika katika chuo
cha VETA-Nyakato jijini Mwanza yakiambatana na maonyesho ya bidhaa na
technolojia mbadala na rafiki kwa Tabaka la Ozoni Pamoja na mafunzo na njia
bora za technologia sahahi ya kuuudumia viyoyozi, majokofu na mitambo ya
kupoozea viwandani
Walengwa wakubwa wa maadhimisho haya ni mafundi wa kuudumia
majokofu viyoyozi mitambo ya kupoozea kutoka viwandani vya kusindika minofu ya
samaki vinywaji na taasisi za ufundi zenye fani ya kuudumia majokofu na
viyoyozi. Lengo kuu ni kuelimisha mafundi kuhusu technolojia mpya.