MAADHIMISHO YA SIKU YA UTALII DUNIANI KITAIFA MKOANI MWANZA TAREHE 23 – 29 SEPTEMBA 2013

Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Uongozi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadau wa tasnia ya utalii nchini wanayo fur... thumbnail 1 summary
Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Uongozi wa Mikoa ya Kanda ya Ziwa pamoja na wadau wa tasnia ya utalii nchini wanayo furaha kuwakaribisha wananchi wote na wadau mbalimbali katika maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka 2013 ambayo Kitaifa yatafanyika Mkoa wa Mwanza.
Siku ya Utalii Duniani huadhimishwa tarehe 27 Septemba ya kila mwaka ambapo kila nchi mwanachama wa Shirika la Utalii Duniani husheherekea siku hii. Kwa mwaka huu Kimataifa, maadhimisho haya yatafanyika katika Visiwa vya Maldives.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Utalii na Maji – Kulinda Hatma Yetu (Tourism and Water – Protecting Our Common Future)”. Kwa kuzingatia kauli mbiu hii, tunawajulisha wadau wote katika nyanja mbalimbali za uhifadhi mazingira, matumizi ya teknolojia sanifu, wafanyabiashara wa tasnia ya utalii na maliasili, wadau wa sekta ya maji, taasisi za elimu, wanasiasa, viongozi na wataalamu mbalimbali kushiriki katika wiki ya maadhimisho ya utalii duniani.
Shughuli zitakazofanyika ni pamoja na tafsiri ya kauli mbiu katika Nyanja mbalimbali kama, mashindano ya uandishi wa insha mbalimbali kuhusiana na mada, michezo na burudani mbalimbali, maonesho ya utalii, malikale, misitu na masuala ya uhifadhi kwa ujumla, teknolojia mbalimbali, pamoja na ziara ya kutembelea Hifadhi ya Saanane.
Wananchi pamoja na wadau wote mnakaribishwa sana kushiriki katika maadhimisho haya.
“Kumbuka Utalii ni nyenzo ya kuhamasisha uhifadhi kwa uhai na ustawi wa Taifa”
Imetolewa na:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Maliasili na Utalii,
S.L.P 9372,
DAR ES SALAAM.
Simu: 255-22-2864230
Barua pepe: ps@mnrt.go.tz