Safari kati ya Arusha na Dar es Salaam yenye umbali wa zaidi
ya kilomita 650 kwa basi inaweza kuchukua zaidi ya masaa 8, umewahi kujiuliza
kwa kutembea kwa miguu unaweza kuchukua muda gani?
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu (anayeongea na simu) akiongoza matembezi ya kupinga ujangili kuelekea mnazi mmoja baada ya kuyapkea Ubungo, kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli na wadau wengine katika mapambano ya ujangili
Lakini uthubutu na nia njema yenye uzalendo ndani
yake ndivyo vilivyowafanya watu 18 washiriki katika matembezi ya kupinga
ujangili nchini "Walk for Elephants"
Matembezi ambayo yamepewa jina la “Walk for
Elephants” yamedumu kwa muda wa siku 19 kabla ya kupokelewa na Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu Alhamisi ya Septemba 12 mwaka 2013.
Nyarandu ameunga mkono uzalendo huo kwa vitendo
pale alipotembea kwa mguu kutoka Ubungo hadi Mnazi Mmoja, akatumia zaidi ya saa
moja na nusu akiambatana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili
na Mazingira, James Lembeli na Mkurugenzi wa idara ya wanyama pori, Profesa Alexander Songorwa pamoja na Mkurugenzi wa African Wildlife Trust, Pratik Patel
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu (katikati), akiwa na wadau wa vita dhidi ya ujangili, Kulia kwake ni Meneja wa maendeleo ya jamii kutoka Friedrikin Group of Comanies, Aurelia Mtui, upande wa kushoto wa Nyarandu ni Faraja Nyarandu na Nancy Sumari pamoja na askari wanyama pori kutoka Arusha.
Nyarandu akaweka
bayana kuwa matembezi hayo ya kupiga vita ujangili nchini yamefanyika wakati
ambapo kuna ongezeko kubwa la ujangili, nchini hususan ujangili wa tembo.
Ujangili ambao unasababishwa
na mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa bei ya meno ya tembo katika
masoko haramu huko Mashariki ya Kati na Asia na Kuimarika na kuongezeka kwa
magenge ya ujangili (poaching syndicates) pamoja na ubora wa mawasiliano.
Sababu nyingine ni Kudorora
kwa uchumi na kuongezeka kwa umasikini katika jamii, hivyo kufanya watu wengi
kujiingiza kwenye ujangili cha uhalifu mwingine, Uroho wa kutaka utajiri wa haraka
haraka ambao umewafanya baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na wadogo na watumishi
wa umma kujiingiza katika ujangili na Rushwa na mmomonyoko wa maadili katika
jamii kwa jumla.
Naibu Waziri, Lazaro Nyarandu akipokea hundi ya dola za kimarekani milioni 250 kutoka kwa Mkurugenzi wa Friedrikin Conservation Fund, Mitchel Allard kwaajili ya kutekeleza shuguhuli za vita dhidi ya ujangili
Ujangili umechangia
sana katika kupungua idadi ya tembo nchini kutoka 350,000 miaka ya 1960 hadi
110,000 mwaka 2009. Idadi ya tembo
wanaouawa na majangili inazidi kuongezeka kila mwaka
Mkurugenzi wa Friedrikin Conservation Fund, Mitchel Allard
Matembezi hayo yameandaliwa na shirika la African
Wildlife Trust yamehitimishwa leo mmnazi mmoja ambapo wadau mbalimbai na wananchi
walifika kuwaona mashujaa waliotembea katika safari hiyo.