Nyota ya Saida Karoli yaanza kung’ara tena, aibuka mshindi tamasha la muziki wa asili

MSANII wa muziki wa asili Saida Karoli juzi ameibuka mshindi katika tamasha la ni nani zaidi, kati ya wasanii wote ambao wamerekodi kazi ... thumbnail 1 summary
MSANII wa muziki wa asili Saida Karoli juzi ameibuka mshindi katika tamasha la ni nani zaidi, kati ya wasanii wote ambao wamerekodi kazi zao katika studio ya Tivol ya jijini Mwanza.

Tamasha hilo lilifanyika katika uwanja wa karume mjini Musoma na kuhudhuriwa na wananchi zaidi ya 5,000 kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo.

Murugenzi mtendaji wa studio ya Tivol, Nilivinus Madaraka, jana alisema kuwa katika tamasha hilo, Saida Karoli aliibuka mshindi, akifuatiwa na Bhudagala Mwanamalonja na nafasi ya tatu ilishikiliwa na Papaa Kishapu.

Madaraka alisema kuwa tamasha hilo lilishirikisha wana muziki 16 ambao wote kazi zao zimerekodiwa katika studio yake na kwamba lengo lake lilikuwa ni kuutangaza muziki wa asili na kuenzi mila na utamaduni wa mtanzania.

Aidha, alisema uwa katika tamasha hilo wasanii walipiga miziki ya asili ili kudumisa utamaduni na mila za mtanzania na kwamba kulingana na idadi kubwa ya watu walioingia zilipatikana zaidi ya shilingi milioni nane.


Alisema kuwa jumamosi ijayo Saida Karoli atatumbuiza katika mji wa Bukoba kwenye ukumbi wa Linaz Club na jumapili atakuwa kwenye uwanja wa Kaitaba mjini humo.