Wakati wa shughuli zangu Mkoani Morogoro miaka kadhaa iliyopita, siku moja nilitamani sana kufika
Ziwa Manyara kuwaona simba wanaopanda miti, nilipiga picha ya umbo lao na namna
wanavyoweza kupanda miti na kuifanya hifadhi hiyo kuwa na sifa ya kipekee
nchini.
Hivyo nilifungasha
safari hadi Manyara na kujionea maajabu hayo. Lakini nilichokiona miaka hiyo
Manyara hivi karibuni nimekiona tena kwenye hifadhi ya taifa ya Mikumi,
kimenifurahisha na kunifanya nikuhabarishe na wewe kwamba kizazi kipya cha
simba wa mikumi nao wanapanda miti.
Kama mawazo yako
yanakutuma kupanda mtini kama njia ya kumkimbia simba wa Mikumi atakaekuvamia,
pole ndugu, atakufuata juu kwa juu.
Kwa wale akina
Thomaso, ambao hawaamini bila kuona wala kugusa, nimekuletea picha 10
zikionyesha simba waki-enjoy na kufanya madoido kadhaa juu ya mti
www.tabianchi.blogspot.com