Prince William, David Beckham na Yao Ming waanzisha kampeni ya kupambana na ujangili ‘United for Wildlife’

Kama hadi sasa hujaamini kuwa ujangili ni janga la dunia naamini hatua ya Mtoto wa Mfalme Prince William kumwomba mchezaji David Beckham ku... thumbnail 1 summary
Kama hadi sasa hujaamini kuwa ujangili ni janga la dunia naamini hatua ya Mtoto wa Mfalme Prince William kumwomba mchezaji David Beckham kuungana naye katika kupambana na ujangili na biashara ya wanyamapori itakufanya upate picha kamili.

Beckham alipoombwa kushirika katika kampeni hiyo ambayo imepewa jina la United for Wildlife hakuwa na kipingamizi na hivyo kuwekwa kwenye list ya watu mashuhuri watakaoshirika kampeni hiyo ambayo inafanyika chini ya usimamaizi wa foundesheni ya ufamle (Rayal Foundation) ambayo mbali na mambo mengine kazi yake ni kupinga ujangili na biashara ya nayara za wanyamapori.

Siku moja tu baada ya kutangaza kuacha kutumikia jeshi Prince Williams ameweka wazi kampeni yake ya kupinga ujangili aliyoipa jina la United for Wildlife ambayo itashirikisha pia taasisi kubwa na zenye ushawishi mkubwa ulimwenguni kwenye masuala ya vita dhidi ya ujangili

Taasisi hiyo itajikita zaidi katika kukomesha biashara haramu ya wanyamapori na zana zake, na itampa muda mwingi Prince William kuitumikia baada ya kumaliza miaka saba katika jeshi.

Prince William ambaye ndiye rais wa taasisi hiyo mpya wiki hii aliungana na Beckham na Mchezaji wa zamani wa basket kutoka China Yao Ming kurekodi video mbili za kupinga biashara haramu ya wanyamapori ikiwa ni msaada kwa taasisi ya kupambana na ujangli na biashara ya ujangili ya WildAid.

Video hizo ambazo zitaonyeshwa hivi karibuni zinalenga kufikisha ujumbe kwenye nchi za mashariki ya mbali na China ambako kuna soko kubwa la bidhha zinazotokana na wanyamapori zilizozuiliwa hasa za tembo na faru.

Inakadiriwa kuwa tembo 25,000 huuawa kila mwaka na majangili wakati faru 618 wameshauawa kwa mwaka huu pekee na kuweka hali ya hatari ya kupotea kwa viumbe hao katika miaka michache ijayo.

Beckham anasema: “Nilipoambiwa kiwango cha ujangili barani Afrika, nilikubali moja kwa moja ombi la Prince William la kufikisha ujumbe huu wa kupinga ujangili, inasikitisha na kushangaza kutambua kuwa kumbe tunaweza kuwakosa wanyama hawa katika kipindi cha uhai wetu”

Lakini kwake Yao Ming, mmoja wa wanamichezo wakubwa kutoka China anasema: "Ni lazima tupunguze (China) mahitaji kama tunataka kuwanusuru wanyamapori hawa, tulifanikiwa kuzuia biashara ya nyangumi ambapo sasa biashara hiyo imepungua na kufikia asilimia 50 hivyo naamini Serikali ya China inaweza kufanya hivyo hata kwa biashara ya meno ya tembo na pembe za faru”

Prince William akizungumzia uanzishwaji wa umoja huo United for Wildlife anasema: “Tishio la kupotea kwa urithi wetu wa asili ni kubwa lakini naamini ushirikiano huu tuliouanzisha utachochea harakati njema za kulinda viumbe hai na wanyama waliokatika athari kwa ajili ya kizazi kijacho”

"Mzizi wa ujangili na biashara haramu ya wanyamapori ni soko, hasa pale unapoona soko linahitaji malighafi ambayo ili ipatikane lazima maelfu ya wanyama hao wauawe, jambo linalowaangamiza na kufanya wapotea ulimwenguni katika kipindi kifupi kijacho”

Anasema kuwa ni lazima kutumia muda huu kufanya kazi pamoja kulinda rasilimali hizo ili kutoa fursa kwa watoto wanaozaliwa leo kuwaona wanyama hao na kufurahia urithi huo ambao kila mtu mwenye mapenzi mema angependa kuendela kuuona.


Taasisi saba zilizoungana na taasisi ya Royal Foundation katika kutekeleza program ya United for Wildlife ni pamoja na Conservation International, Fauna & Flora International, International Union for Conservation of Nature, The Nature Conservancy, Wildlife Conservation Society, WWF-UK na taasisi ya Zoological Society ya London.